DOZI HII WAMEANDALIWA WAZAMBIA WA SIMBA

KOCHA Mkuu wa Simba, Pablo Franco, raia wa Hispania, amefichua malengo yao makubwa kwa sasa ni kuhakikisha wanawaondoa wapinzani wao katika Kombe la Shirikisho Afrika, Red Arrows ya Zambia kutokana na maandalizi makubwa wanayoyafanya kwa sasa. Simba inatarajia kucheza na Red Arrows ya Zambia katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika kesho Jumapili kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar. Pablo ametoa kauli hiyo kuelekea mchezo wa kwanza wa…

Read More

YACOUBA KUKOSEKANA YANGA MSIMU MZIMA

LICHA ya mafanikio makubwa ya upasuaji wa goti aliofanyiwa kiungo Mburkinabe wa Yanga, Yacouba Songne, imeelezwa kuwa kiungo huyo yupo hatarini kukosa michezo iliyosalia ya msimu huu kutokana na kuuguza jeraha hilo. Yacouba alipata majeraha hayo ya goti kwenye mchezo dhidi ya Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam, ambapo upasuaji wake ulifanyika Novemba 11, mwaka huu. Yacouba tayari amerejea nchini…

Read More

SIMULIZI YA ALIYEACHWA KISA MKWANJA

SIMULIZI ya aliyeachwa kisa ishu ya mkwanja Tuiishi pamoja na mume wangu Kibet katika kaunti ya Lamu ambapo nilifanya kazi ya udaktari katika hospitali moja ya kibinafsi katika kaunti ile. Mume wangu naye alifanya kazi ya uhandisi katika wizara ya ujenzi kwenye kauti ile. Maisha yetu yalikuwa ya kutamaniwa kwani hakuna wakati hata mmoja tuligombana…

Read More

RONALDINHO ANUKIA JELA ISHU YA MAPENZI

NYOTA wa zamani wa timu ya taifa ya Brazil na Klabu ya Barcelona na AC Milan, Ronaldinho ameonywa kwamba anaweza kuibukia jela ikiwa atashindwa kumlipa mgawo wa mali mpenzi wake wa zamani ifikapo Desemba Mosi mwaka huu. Taarifa kutoka nchini Brazil zimeeleza kuwa nyota huyo mwenye miaka 41 ametakiwa kumaliza ishu hiyo na Priscilla Coelho…

Read More

STERLING KUSAINI DILI JIPYA CITY

MANCHESTER City wana imani kubwa ya kumpa dili jipya nyota wao Raheem Sterling ili aweze kuendelea kuitumikia timu hiyo kwa kuwa dili lake linakaribia kumeguka na yeye ameanza kuwa kwenye ubora. Kiungo huyo alianza msimu wa 2021/22 vibaya ambapo aliweza kucheza mechi nne kisha akaweka wazi kwamba anahitaji kuondoka ndani ya kikosi hicho kinachonolewa na…

Read More

MABOSI SIMBA WAMUWEKEA MTEGO PABLO

WAKATI kesho Pablo Franco akiwa na kibarua cha kusaka ushindi mbele ya Red Arrows katika mchezo wa kimataifa wa Kombe la Shirikisho, mabosi wa Simba wamempa mtego kocha wao kwa kumpa malengo makubwa ambayo anapaswa kuyafikia. Pablo amerithi mikoba ya Didier Gomes ambaye aliomba kuondoka baada ya timu hiyo kuboronga katika Ligi ya Mabingwa Afrika…

Read More

SIMBA YAIPIGIA MATIZI RED ARROWS KWA MKAPA

PABLO Franco, leo Novemba 26 ameongoza mazoezi kwa mara ya kwanza kwa kikosi chake katika Uwanja wa Mkapa. Mazoezi ya leo ni kwa ajili ya mchezo wa Kombe la Shirikisho ambao ni wa mtoano na unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa. Itakuwa ni Novemba 28 ambapo mashabiki 35,000 wa Simba wameruhusiwa kuingia kushuhudia mchezo huo. Kwa…

Read More

RED ARROWS WAPINZANI WA SIMBA WANA MCHECHETO

WAPINZANI wa Simba katika Kombe la Shirikisho barani Afrika, Klabu ya Red Arrows imeweka wazi kuwa nia yao ya kusonga mbele katika michuano hiyo huku wakitamba kufanya vizuri wakiwa ugenini. Red Arrows kutoka Zambia Jumapili Novemba 28 watacheza mchezo wao wa kwanza wa mtoano wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Simba kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar. Mchezo wa marudiano unatarajiwa kufanyika Desemba Mosi nchini Zambia ambapo Simba watakuwa ugenini…

Read More

KOCHA HUYU HAPA KUIBUKIA MANCHESTER UNITED

RALF Rangnick mwenye umri wa miaka 63 anatarajiwa kupewa majukumu ya kuwa Kocha Mkuu kwa muda ndani ya kikosi cha Manchester United akichukua mikoba ya Ole Gunnar Solskjaer ambaye alichimbishwa ndani ya kikosi hicho. Rangnick atapaswa kuweka kando majukumu yake aliyokuwa akiyafanya ndani ya Lokomotiv Moscow ili kuweza kumpokea kocha wa mpito, Michael Carrick ambaye…

Read More

MASHABIKI RUKSA MECHI YA SIMBA V RED ARROWS KWA MKAPA

MASHABIKI 35,000 ni ruksa kuushuhudia mchezo wa Kombe la Shirikisho ambao unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa, Novemba 28. Kwa mujibu wa Shirikisho la Soka Afrika, (CAF) ni mashabiki hao wataruhusiwa kuwa ndani ya uwanja kushuhudia mchezo huo. Na pia mashabiki hao wanapaswa kufuata taratibu na kanuni za kujilinda dhidi ya Corona. Unatarajiwa kuwa mchezo mkali…

Read More

MOLOKO NDANI YA YANGA AHUSIKA KATIKA MABAO MAWILI

JESUS Moloko ndani ya Yanga kwa msimu wa 2021/22 amehusika katika mabao mawili kati ya mabao 10 ambayo yamefungwa. Ametupia mabao mawili katika ligi akitumiq pasi ya mshambuliaji wa Yanga, Yacouba Songne raia wa Burkina Faso. Kwa sasa Yacouba yupo nje ya uwanja akipata matibabu zaidi baada ya kupata majeraha alipokuwa akitumikia timu hiyo kwenye…

Read More

MANCHESTER CITY YAICHAPA PSG NA MESSI NDANI

MBELE ya mastaa wakubwa ambao wanalipwa mkwanja mrefu ikiwa ni pamoja na Lionel Messi, Neymar Jr na Kylian Mbappe bado Manchester City waliibuka wababe. Ni katika mchezo uliochezwa Uwanja wa Etihad ambao ulikuwa ni wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, City walisepa na pointi tatu mazima. Ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya PSG unaifanya timu hiyo…

Read More