Yanga SC Yamuuza Allan Okello FAR Rabat
Klabu ya Yanga SC imekubali kumuuza winga wake wa kimataifa wa Uganda, Allan Okello, kwenda…
Klabu ya Yanga SC imekubali kumuuza winga wake wa kimataifa wa Uganda, Allan Okello, kwenda FAR Rabat ya Morocco kwa ada kubwa ya uhamisho. Okello, ambaye alikuwa sehemu ya kikosi cha Yanga, sasa anaelekea kuanza changamoto mpya katika soka la Morocco baada ya pande hizo kufikia makubaliano ya uhamisho wake. Uhamisho huo unatajwa kuwa wa…
Hatimaye Yanga SC imemtambulisha rasmi kiungo mshambuliaji wa kimataifa wa Burkina Faso, Stephane Aziz Ki, ambaye amerejea Jangwani baada ya kuondoka katika klabu hiyo mwaka 2025. Aziz Ki aliondoka Yanga na kujiunga na Wydad Casablanca ya Morocco, kabla ya baadaye kuhamia Al-Ittihad Tripoli ya Libya. Sasa nyota huyo amerejea Yanga akiwa na historia kubwa ndani…
Manchester United imeanza safari ya kuelekea msimu mpya kwa kichapo cha mabao 4-2 dhidi ya AC Milan katika mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye Tarczyński Arena, Wrocław, Poland. Mchezo huo ulikuwa wa kipekee kutokana na AC Milan kuwa chini ya kocha wa zamani wa Manchester United, Rúben Amorim, ambaye safari hii ameibuka na ushindi dhidi ya…
Klabu ya Simba leo Agosti 15, 2026 imemtambulisha rasmi mshambuliaji Ismail Mgunda kuwa mchezaji mpya wa klabu hiyo kwa ajili ya msimu wa 2026/27. Mgunda, mwenye umri wa miaka 31, amejiunga na Simba akitokea Mashujaa FC kwa mkataba wa miaka miwili. Mshambuliaji huyo raia wa Tanzania anatarajiwa kuongeza nguvu na ushindani katika safu ya ushambuliaji…
Atlanta United ya Marekani iko katika hatua za mwisho kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Uswisi, Breel Embolo, kutoka klabu ya Rennes ya Ufaransa. Kwa mujibu wa The Athletic, Atlanta United imekubali ada ya uhamisho inayokadiriwa kufikia dola milioni 18 sawa na TSh bilioni 46.8, kiasi ambacho kitamfanya Embolo, mwenye umri wa miaka 29,…
Polisi Tanzania FC na Azam FC zimetoka sare ya bao 1-1 katika mchezo wa ushindani uliopigwa leo kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha. Mchezo huo ulikuwa na ushindani mkubwa huku timu zote zikionekana kutafuta nafasi ya kupata bao la kuongoza. Polisi Tanzania ilifanikiwa kuvunja ukuta wa Azam FC dakika ya 74 baada ya kupewa…
Leo Jumamosi, Agosti 15, FC Utrecht watawakaribisha AZ Alkmaar uwanjani Stadion Galgenwaard, jijini Utrecht, katika mechi ya raundi ya pili ya Eredivisie ya Uholanzi. Mechi hii itaanza saa 19:45 usiku. Ni mchezo kati ya timu mbili zenye mwelekeo tofauti mapema kwenye msimu AZ wakiwa juu ya msimamo na Utrecht wakijaribu kujiweka sawa kwenye msimamo baada…
Agosti 15,2026 NBC Premier League inatarajiwa kuendelea mara baada ya pazia kufunguliwa rasmi Agosti 14,2026. Kuna mechi 3 kali zinatarajiwa kuchezwa leo katika viwanja vitatu tofauti ambapo mabingwa watetezi Yanga SC watakuwa ugenini. Polisi Tanzania vs Azam FC, saa 10:00 jioni, Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha. Coastal Union vs Mashujaa FC, saa 12:30 jioni,…
PARIS, Ufaransa — 15 Agosti 2026: Mabingwa wa Ulaya, Paris Saint-Germain (PSG), wamekamilisha usajili wa mshambuliaji wa Barcelona na timu ya taifa ya Hispania, Ferran Torres, kwa mkataba utakaomuweka klabuni hapo hadi mwaka 2031. Torres, mwenye umri wa miaka 26, amejiunga na PSG kwa ada inayoripotiwa kufikia Euro milioni 50 (takribani pauni milioni 42.7), baada…
Uwanja wa kasino umepata mgeni mpya, Bubble Up kutoka Pragmatic Play sasa inapatikana Meridianbet, ikiwa imekuja na mchanganyiko wa rangi, bubbles na mfumo wa uchezaji unaolenga kuwapa wachezaji uzoefu mpya wa kusisimua. Mchezo huo umefunguliwa kwa mashabiki katika kipindi maalum kuanzia Agosti 10 hadi Agosti 24, 2026. Hii ni fursa kwa wachezaji kuonja mchezo kabla…
Pamba Jiji na Dodoma Jiji zimeanza msimu wa Ligi Kuu ya NBC 2026/27 kwa kugawana alama baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika mchezo wa ufunguzi uliochezwa leo, Agosti 14, 2026, kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza. Dodoma Jiji ndiyo ilianza kwa kasi katika mchezo huo na kufanikiwa kupata bao la kuongoza dakika ya…
Klabu ya Mashujaa FC ya Kigoma imefanikiwa kumnasa golikipa Wilbol Maseke, aliyekuwa akiitumikia Coastal Union, kwa usajili wa mchezaji huru. Usajili huo unatajwa kuwa hatua muhimu kwa Mashujaa FC katika kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu mpya, hasa katika eneo la ulinzi wa lango ambalo linahitaji uzoefu na utulivu. Maseke anafahamika kwa uwezo wake wa kulinda…
Msimu mpya wa LALIGA 2026/27 unatarajiwa kuanza wikiendi hii, huku mashabiki wa soka nchini Hispania na duniani wakisubiri kwa hamu mwanzo wa mbio mpya za ubingwa. Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa, mchezo wa kwanza wa msimu utakuwa kati ya Racing na Villarreal, utakaochezwa Jumapili, Agosti 16, kuanzia saa 12:00 jioni. Baada ya mchezo huo, Espanyol…
Beki wa Yanga SC, Bakari Mwamnyeto, amesema morali ndani ya kikosi hicho ipo juu kuelekea mchezo wao wa kwanza wa ligi dhidi ya Namungo FC, huku akisisitiza kuwa wamejiandaa kuhakikisha wanaondoka na alama tatu. Yanga inatarajiwa kushuka dimbani Jumamosi, Agosti 15, 2026, kukutana na Namungo FC katika Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa, Lindi, katika mchezo unaotarajiwa…
Pazia la NBC Premier League linatarajiwa kufunguliwa rasmi Agosti 14 huku Simba SC ikiwa na mechi 5 za moto mwanzo wa msimu kusaka pointi 3 muhimu. Simba SC ilimaliza nafasi ya pili kwenye msimamo baada ya mechi 30 ikivuna pointi 73 tofauti ya pointi 2 na mabingwa Yanga SC waliomaliza msimu wakiwa na pointi 75….
HATIMAYE kile kitabu kipya cha Msichana wa Maisha Yangu kutoka kwa Best Seller Authors, Lunyamadzo Mlyuka kimepandishwa leo Agosti 14,2026 kwenye mtandao wa mauzo wa selar.com. Hii ni njia nyingine tena kwa msomaji kupata kitabu chenye simulizi ya kiafrika inayozungumzia maisha halisi na mabadiliko ya teknolojia. Kuipata sasa bofya hapa: Buy Book: Msichana wa Maisha…
Yanga SC inayonolewa na Kocha Mkuu Manqoba Mngqithi, ilimaliza msimu wa 2025/26 ikiwa na pointi 75 baada ya mechi 30, ilipoteza mchezo mmoja pekee dhidi ya Dodoma Jiji FC. Kwa sasa timu hiyo ipo Lindi kwa maandalizi ya mchezo wa ufunguzi ndani ya msimu mpya wa 2026/27 unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Majaliwa. Ni Agosti 15…