KOCHA AZAM FC AIBUKIA BIASHARA UNITED

BIASHARA United imemtambulisha rasmi Vivier Bahati kuwa kocha mkuu wa timu hiyo na tayari ameanza kazi rasmi kuinoa timu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu Bara. Bahati alikuwa anainoa timu ya Azam FC mkataba wake ulivunjwa kutokana na mwendo mbovu wa timu hiyo na waliondoka pamoja na Kocha Mkuu, George Lwandamina. Anachukua mikoba ya Patrick Odhiambo ambaye…

Read More

FT:MBUNI FC 0-2,MUKOKO ATUPIA MBILI

UWANJA wa Sheikh Amri Abeid dakika 90 zimekamilika kwenye mchezo wa kirafiki kati ya Yanga na Mbuni ambapo ni Yanga wameibuka kidedea kwenye mchezo wa leo. Mabao yote ya Yanga yamefungwa kipindi cha pili kwa kuwa dakika 45 za mwanzo timu zote zilitoshana nguvu na mtupiaji ni Mukoko Tonombe ambaye alifunga mabao hayo kwa penalti…

Read More

MCHEZO WA KIRAFIKI, YANGA 0-0 MBUNI FC

MCHEZO wa kirafiki kati ya Yanga v Mbuni kwa sasa ni mapumziko Uwanja wa Sheikh Amri Abeid. Mchezaji wa Mbuni Hussein Idd ameonyeshwa kadi nyekundu kipindi cha kwanza baada ya kumchezea faulo mchezaji wa Yanga David Bryson. Kiungo mshambuliaji Dickosn Ambundo alifanya jaribio la kwanza na matata kwa upande wa Yanga lakini liliokolewa na kipa…

Read More

KIKOSI CHA YANGA DHIDI YA MBUNI FC

LEO kikosi cha Yanga kinacheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Mbuni FC Uwanja wa Sheikh Amri Abeid kwa ajili ya kujiweka sawa kuelekea mchezo wao dhidi ya Polisi Tanzania. Hiki hapa kikosi cha kwanza:- Johora Boxer Bryson David Mukoko Ibrahim Bacca Zawad Mauya Sure Boy Ambundo Farid Mussa Kaseke Makambo Benchi Magaigwa Job Balama Moloko…

Read More

GHANA WAONDOLEWA AFCON

TIMU ya Taifa ya Ghana imeondolewa rasmi kwenye mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika AFCON 2021 na timu ya taifa ya Comoros katika mchezo wa mwisho wa Kundi C kwa kipigo cha mabao 3-2 katika mchezo uliopigwa Jumanne Januari 18. Ghana ni washindi wa Kombe la Afcon mara nne wametolewa na timu ambayo ni…

Read More

ISHU YA KUBEBA MATOKEO MFUKONI IWEKWE KANDO

KILA mmoja kwa sasa kwenye ligi anavuna kile ambacho alikipanda wakati wa maandalizi na hakuna bahati mbaya ambayo inatokea. Ikumbukwe kwamba ni muda mfupi tumetoka kukamilisha dirisha dogo la usajili ambalo lilikuwa lina mambo mengi na sarakasi za kutosha mwisho wa siku kila kitu kimekuwa wazi. Ilikuwa namna hiyo kwa wale ambao walikuwa wanahitaji kufanya…

Read More

YANGA KUTESTI MITAMBO LEO

VINARA wa Ligi Kuu Bara Yanga leo watakuwa na kazi ya kutesti mitambo kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Mbuni FC. Saa 10:00 jioni mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid ikiwa ni kwa ajili ya hesabu za mchezo wao ujao dhidi ya Polisi Tanzania ambao ni wa ligi. Januari 23 Yanga yenye…

Read More

SIMBA KITUO KINACHOFUATA MANUNGU

BAADA ya kurejea Dar wakitoka Mbeya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara kituo chao kinachofuata ni Manungu. Chini ya Kocha Mkuu, Pablo Franco, Januari 17,2022 alishuhudia ubao wa Uwanja wa Sokoine ukisoma Mbeya City 1-0 Simba na mtupiaji alikuwa ni Paul Nonga dakika ya 19. Unakuwa ni mchezo wa kwanza kwa timu hiyo kupoteza ndani…

Read More

AZAM WASEPA NA POINTI TATU ZA MBEYA KWANZA

Rodgers Kola amepachika bao mbele ya Mbeya Kwanza katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa Uwanja wa Sokoine. Bao hilo la ushindi amelipachika kimiani dakika ya 44 katika kipindi cha kwanza. Jitihada za Mbeya Kwanza kuweza kuweka mzani sawa ziligonga mwamba katika dakika 45 za kipindi cha kwanza. Hata kipindi cha pili mambo yalikuwa magumu…

Read More

MORRISON AFUGUKIA ISHU YA KUSUGUA BENCHI

KIUNGO Mshambuliaji wa Simba, Bernard Morrison, amefunguka kuwa, hana shida na kuanzia benchi ndani ya kikosi hicho, kwani ni jambo la kawaida kwenye timu yoyote kubwa na wajibu wake kama mchezaji ni kuhakikisha anaongeza jitihada kumshawishi kocha kumpa nafasi. Tangu kiungo raia wa Senegal, Pape Sakho aanze kuuwasha moto ndani ya Simba, Morrison ameonekana kupata…

Read More

LEWANDOWSKI,RONALDO WASEPA NA TUZO

MSHAMBULIAJI wa kimataifa kutoka Poland ambaye anakipiga Bayern Munich, Robert Lewandowski ameshinda tuzo ya FIFA ya Mchezaji Bora wa mwaka 2021. Lewandowski, 33, ametwaa tuzo hiyo ikiwa ni mara ya pili mfululizo ambapo katika kipindi hicho ametupia bao 69 akimshinda Lionel Messi na Mohamed Salah wa Liverpool. Pia mshambuliaji wa Manchester United Cristiano Ronaldo yeye…

Read More

SIMBA YATAJA TIMU ITAKAYOTWAA UBINGWA

KOCHA wa Simba, Pablo Franco amesema kuwa kwa upande wako anaona Azam FC wanayo nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa kwa siku za mbeleni kutokana na kikosi chao kuimarika kila siku. Pablo amesema amekutana na Azam FC kwenye mechi mbili kwa siku za hivi karibuni na ameona kuna utofauti mkubwa kwenye mechi ya kwanza na ya pili ambayo wamecheza na anaona kabisa timu ina ari ya…

Read More

LIGI KUU BARA KUENDELEA MBEYA,PALEPALE SOKOINE

 LEO Januari 18 kutakuwa na mchezo mmoja wa Ligi Kuu Bara ambapo Mbeya Kwanza itawakaribisha Azam FC kwenye mchezo unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Sokoine. Itakuwa ni saa 10:00 jioni, ambapo uwanja huo jana ulitumika kwa Mbeya City kuweza kuitungua Simba bao 1-0 ambalo lilifungwa na Paul Nonga dakika ya 19. Mbeya Kwanza iliyo nafasi ya…

Read More

KIUNGO MPYA WA YANGA HESABU ZAKE KUBWA KWELI

CHICO Ushindi kiungo mpya ndani ya kikosi cha Yanga ameweka wazi kwamba hesabu kubwa baada ya kuwa ni mali ya Yanga ni kuweza kuipa ushindi timu hiyo kwenye mechi ambazo watacheza. Ushindi ni moja ya usajili mpya kwenye dirisha dogo na alitambulishwa Tanga, Uwanja wa Mkwakwani wakati ubao uliposoma Coastal Union 0-2 Yanga. Kiungo huyo…

Read More