TORRES NI MALI YA BARCELONA

Nyota wa kimataifa wa Hispania Ferran Torres amekamilisha dili lake la kujiunga na FC Barcelona akitokea Manchester City dili linalotajwa kuwa na thamani ya pauni milioni 61. Torres mwenye umri wa miaka 21, anarejea Hispania baada ya miezi 18 tangia aondoke Valencia na kujiunga na Manchester City ambapo sasa ameingia mkataba wa miaka sita (2027)…

Read More

RUDIGER APELEKWA MAN U

BEKI wa zamani wa Manchester United Paul Parker anaamini kama beki wa Chelsea, Antonio Rudiger angetua kikosini hapo basi huenda angekuwa msaada mkubwa. Nyota huyo kuelekea Januari mwakani atakuwa huru kuzungumza na timu yoyote ambayo itakuwa inahitaji huduma yake. Mkataba wake ndani ya Chelsea kwa sasa upo ukingoni kumeguka na mabosi wa timu hiyo nao…

Read More

SALAH ATAMWAGA WINO LIVERPOOL

JURGEN Klopp, Kocha Mkuu wa Liverpool amesema kuwa anaamini kwamba nyota wake Mohamed Salah atasaini tena mkataba mpya. Ni miezi 18 imesalia kwa Salah kubaki ndani ya Liverpool ambapo amekuwa akitajwa kwamba anaweza kusepa Anfield. Ilielezwa kuwa tayari Liverpool wameanza mazungumzo na raia huyo wa Misri ambaye amekuwa na ushkaji mkubwa na kucheka na nyavu…

Read More

HONGERA KOMBA,WENGINE WAJIFUNZE

KWA ambalo limetokea kwa waamuzi wa Tanzania bado kuna jambo la kujifunza ili wakati ujao orodha ya majina ya waamuzi ambao watapewa nafasi ya kuchezesha mashindano ya kimataifa izidi kuongezeka. Mwamuzi Mtanzania, Frank Komba ni yeye pekee ambaye ameweza kupenya kwenye orodha hivyo katika hilo kuna jambo la kujifunza. Kwa Komba kuteuliwa na CAF kuwa…

Read More

LUIS MIQUISSONE ABEBA SUPER CUP AFRIKA

LUIS Miquissone nyota wa zamani wa Simba anaingia katika rekodi ya wachezaji waliosepa na taji la Super Cup baada ya timu yake mpya kushinda. Mchezo uliochezwa Uwanja wa Al Rayyan miamba Al Ahly na Raja Casablanca walitoshana nguvu kwa kufungana bao mojamoja ambapo kwa Al Ahly Taher Mohamed alisawazisha bao dakika ya 90 ambalo Yasser…

Read More

SALAH HANA JAMBO DOGO ULAYA

MOHAMED Salah raia wa Misri, mshambuliaji wa Liverpool hana jambo dogo akiwa uwanjani kwa kuwa amekuwa ni mtu wa kazikazi. Rekodi zinaonyesha kuwa amecheza jumla ya mechi 162 na ni mechi 155 alianza kwenye kikosi cha kwanza. Katika mechi hizo jumla ya mechi saba alifanyiwa mabadiliko kutokana na sababu mbalimbali. Akiwa ametupia mabao 110 ni…

Read More

GUARDIOLA AWAPA ONYO MASTAA WAKE

PEP Guardiola, Kocha Mkuu wa Manchester City amewapa onyo mastaa wake Jack Grealish na Phil Foden kutokana na tabia zao za kupenda bata wakati wanajua kwamba wanamajukumu kwenye timu. Nyota hao wawili walishinda klabu usiku wakati wakijua kwamba kuna mchezo dhidi ya Newcastle United hali iliyopelekea kutoweza kupangwa kwenye mchezo huo. Wakati City ikishinda mabao…

Read More

AFCON IPO KAMA KAWAIDA

SHIRIKISHO la soka barani Afrika, (CAF) limethibitisha kuwa fainali za kombe la Mataifa ya Afrika AFCON 2022 zitafanyika nchini Cameroon kama ilivyokuwa imepangwa awali. Hii inafuatia wiki kadhaa za mikwara na miongozo ya UEFA na FIFA kutaka AFCON isogezwe mbele. Na sasa ni rasmi maombi hayo yamegonga mwamba na CAF chini ya Rais Patrice Motsepe…

Read More

RUDIGER KUKUNJA MKWANJA MREFU REAL MADRID

IKIWA dili lake litakamilika kujiunga na kikosi cha Real Madrid akitokea Klabu ya Chelsea basi beki Antonio Rudiger atakunja mkwanja mrefu kweli. Rudiger anatarajiwa kuondoka kwenye kikosi hicho na timu kadhaa Ulaya zinatajwa kuwania saini yake. Ambao wapo mbele kuwania saini ya mwamba huyo ni Real Madrid ambao wao wametenga kabisa kitita cha mshahara wa…

Read More

MANCHESTER UNITED YAOMBWA MECHI KUPELEKWA MBELE

KLABU ya Manchester United imeomba Ligi Kuu ya Uingereza kuahirisha mchezo wa leo dhidi ya Brentford baada ya kulazimika kusitisha mazoezi ya kikosi chake cha kwanza Desemba 13 kotokana na Corona. Kitabu cha mwongozo cha Ligi Kuu ya 2021/22 kinajumuisha itifaki za UVIKO-19, na kinaruhusu bodi ya Ligi Kuu kupanga upya au kuahirisha mechi ya…

Read More

AUBA MAJANGA,AVULIWA UNAHODHA

KLABU YA Arsenal inayoshiriki Ligi Kuu England imemvua unahodha Pierre-Emerick Aubameyang na hatacheza kwenye mechi ya ligi dhidi ya West Ham kesho Jumatano usiku. Raia huyo wa Gabon kwake inakuwa ni majanga kuvuliwa kitambaa hicho pamoja na mwendo wake kuwa wa kusuasua kwa msimu wa 2021/22. “Kufuatia ukiukaji wake wa nidhamu wiki iliyopita, Pierre-Emerick Aubameyang…

Read More