
MUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA SPOTI XTRA ALHAMISI
MUONEKANO wa ukurasa wa mbele gazeti la Spoti Xtra Alhamisi
MUONEKANO wa ukurasa wa mbele gazeti la Spoti Xtra Alhamisi
UWANJA wa Azam Complex, dakika 90 za zimekamilika na Yanga inasepa na pointi tatu muhimu ikiwa ugenini. Vinara hao wa ligi wanafikisha pointi 51 wamepindua meza kibabe baada ya kuanza wakiwa wanadaiwa bao moja kisha wakalipa na kuogeza bao lingine la ushindi. Azam FC wanapaswa wajiliamumu wenyewe kwa kuwa walikosa nafasi za wazi tatu za…
KIKOSI cha Yanga kinachotarajiwa kuanza leo Aprili 6 Uwanja wa Azam Complex dhidi ya Azam FC. Ngoma inapigwa saa 2:15, tayari kikosi cha Yanga kimewasili Uwanja wa Azam Complex na wachezaji walipita mlango ule wa mashabiki
WASHINDI watatu Shaaban Mwita wa Mgusu (Geita), Abdalla Said Ali wa Tandahimba (Mtwara) na David Jonas wa Magu (Mwanza), leo asubuhi wameibuka washindi wa vitita vya shilingi milioni moja moja kila mmoja katika droo ya nne ya wiki ya Bet Bonanza ya SportPesa. Droo hii ni sehemu ya promosheni ya Bet Bonanza ya SportPesa, na…
MFUMO ni uleule wa kusaka ushindi kwa timu zitakazoshuka uwanjani na hii ya leo ni Dabi ya Dar es Salaam itakayopigwa Uwanja wa Azam Complex saa 2:15 usiku. Unaambiwa acha inyeshe tuone panapovuja baada ya dakika 90 itafahamika nani ni nani kati ya Azam FC v Yanga. Timu zote zina wakali wa kucheka na nyavu…
TAARIFA zilizothibitishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Klabu ya Soka ya Simba Barbara Gonzalez ni kuwa kiungo mshambuliaji wa klabu hiyo Bernard Morrison hawezi kuingia ndani ya ardhi ya Afrika Kusini kutokana na kuwa na kizuizi cha kuingia nchini humo. Morrison kabla ya kujiunga na vilabu vya Yanga na Simba tayari alishawahi kufanya kazi nchini Afrika…
ZOTE mbili ni za moto kwa sasa kwa kuwa zimetoka kushinda mechi zao zilizopita na kujiwekea pointi tatu kibindoni. Ni Azam FC iliyotoka kushinda kwa mabao 2-1 dhidi ya Namungo FC kwenye mchezo uliochezwa Uwanja wa Ilulu na Yanga iliyotoka kushinda mabao 2-0 dhidi ya KMC Leo wana kazi ya kusaka pointi tatu muhimu kwenye…
PABLO Franco, Kocha Mkuu wa Simba ametwaa tuzo ya Kocha Bora ndani ya Ligi Kuu kwa mara ya kwanza baada ya kupewa dili na Simba akichukua mikoba ya Didier Gomes. Kwa mujibu wa Kikao cha Kamati ya Tuzo ya Shirikisho la Soka Tanzania,(TFF) kilichokaa hivi karibuni kimetoa mapendekezo ya jina la Pablo wa Simba. Ametwaa…
CLATOUS Chama kiungo mshambuliaji wa kikosi cha Simba amechaguliwa kuwa mchezaji bora kwa mwezi Machi. Kwa mujibu wa Kikao cha Kamati ya Tuzo ya Shirikisho la Soka Tanzania, (TFF) kilichokutana mwanzo mwa juma hili kimetoa mapendekezo hayo. Chama ameweza kutimiza majukumu yake vema katika mechi mbili ambazo aliweza kufunga mabao mawili na Simba ikaweza kusepa…
NYOTA wawili wa Simba, Bernard Morrison na Chris Mugalu kwenye mashindano ya kimataifa ni habari nyingine kwa kuwa wameweza kufanya maajabu kwenye mechi ngumu kwa kushirikiana na wachezaji wengine. Morrison kwenye mashindano ya kimataifa kuanzia hatua ya mtoano ametumia dk 290 katupia mabao matatu na pasi mbili za mabao. Chris Mugalu yeye amecheza mechi tatu…
SENZO Mbatha, Mtendaji Mkuu Klabu ya Yanga ameweka wazi kuwa Fiston Mayele atafunga mabao mengi msimu huu. Mayele ni mshambuliaji namba moja ndani ya kikosi hicho akiwa ametupia mabao 10 na pasi tatu za mabao. Kiongozi huyo amesema kuwa kutokana na kasi ya Mayele pamoja na mechi ambazo zipo mbele atafunga zaidi ya mabao aliyonayo…
HATUA moja kila wakati hasa kwa wawakilishi wetu wa Tanzania kwenye mechi za kimataifa baada ya kuweza kutimiza lengo la kufika hatua ya robo fainali. Tulizungumza hapa kwamba haitakuwa kazi nyepesi kwa kuwa wapinzani wao USGN hawakuwa na cha kupoteza na ilikuwa hivyo kwa kuwa walicheza mchezo ambao ulikuwa ni wa tofauti. Dakika 45 za…
NI Aprili 6 Ligi Kuu Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea ambapo mechi mbili zinatarajiwa kuchezwa kwenye viwanja viwili tofauti kwa timu kusaka pointi tatu muhimu. Uwanja wa Karume, Mara unatarajiwa kuchezwa mchezo kati ya Biashara United v Mbeya Kwanza ya kutoka Mbeya. Biashara United imekusanya pointi 19 inakutana na Mbeya Kwanza yenye pointi 14 zote zimecheza…
PABLO Franco, Kocha Mkuu wa Simba amesema kuwa wapinzani wao kimataifa katika hatua ya robo fainali ambao ni Orlando Pirates wana wasiwasi kutokana na kupangwa na timu bora. Jana Aprili 5 nchini Misri ni droo ya mechi za kimataifa ambapo Simba imepangwa kucheza na Orlando Pirates ya Afrika Kusini. Simba iliweza kutinga hatua ya robo…
WAKIWA Uwanja wa City of Manchester waliweza kupata ushindi wa bao 1-0 Atletico Madrid ikiwa ni mchezo wa UEFA Champions League. Huu ni mchezo wa kwanza robo fainali na mtupiaji alikuwa ni Kevin De Bruyne ilikuwa dk ya 70. City iliweza kuwa imara kila idara mwanzo mwisho katika mchezo huo licha ya Atletico Madrid kupaki…
KOCHA Mkuu wa Klabu ya Azam Abdi Hamid Moallin amekubali ubora wa kikosi cha Yanga na kuweka wazi kwamba anaandaa mbinu ili kuwakabili vinara wa Ligi Kuu Bara. Moallin amesema kuwa anatambua kwamba wameachwa kwa pointi nyingi na wapinzani hao ambao wanaongoza ligi kwa wakati huu. “Ninatambua kwamba Yanga ni timu imara na inaongoza ligi…