>

KOCHA SIMBA ASAINI KMC

HITIMANA Thiery amesaini dili la mwaka mmoja kuinoa Klabu ya KMC inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara. Kocha huyo hivi karibuni alisitisha mkataba wake na Klabu ya Simba ambayo inanolewa na Kocha Mkuu, Pablo Franco. Alijiunga na Simba kwa ajili ya mashindano ya kimataifa kwa kuwa aliyekuwa kocha wa wakati huo Didier Gomes hakuwa na vigezo…

Read More

MTIBWA WAANZA KUIWINDA RUVU

OFISA Habari wa Mtibwa Sugar, Thobias Kifaru, ameweka wazi juu ya maandalizi yao kuelekea mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Ruvu Shooting utakaochezwa Januari 14, mwaka huu kwenye Uwanja wa Mabati, Pwani.   Mtibwa Sugar ikiwa na kumbukizi nzuri ya kutoka kuichapa Costal Union 1-0, inashika nafasi ya 13 kwenye msimamo wa Ligi Kuu…

Read More

DSTV YAFUNGUA MWAKA NA PANDA TUKUPANDISHE!

Mwaka 2022 unaanza na habari njema kwa wateja wa DStv! Kuanzia tarehe 5 Januari 2022, DStv itaanza promosheni yake kabambe ijulikanayo kama ‘Panda Tukupandishe’ ambapo wateja wa DStv watapatiwa vifurushi vya juu ili kufurahia zaidi burudani katika kipindi hiki cha mwanzo wa mwaka.   Promosheni hii itadumu kwa miezi mitatu na ni kwa wateja wa…

Read More

MZAMBIA HUYU AINGIA ANGA ZA SIMBA NA YANGA

  MOSES Phiri, mshambuliaji wa Zanaco FC ya Zambia anatajwa kuzichonganisha timu kongwe Bongo, Simba na Yanga ambazo zote zinatajwa kuisaka saini yake. Nyota huyo anatajwa kwamba amezungumza na mabosi wa Simba ambao wanahitaji huduma yake ila kabla hajamwaga wino na Yanga nao wanatajwa kubisha hodi. Mambo yamebadilika kwa sasa na ushindani wa kuisaka saini…

Read More

USAJILI UFANYWE KWA UMAKINI MKUBWA

ILIKUWA ni Desemba 16 baada ya dirisha dogo la usajili kufunguliwa na sasa ni Januari 6 mambo yanazidi kwenda kasi huku vurugu za usajili zikiendelea. Ule usemi wa mwenye kisu kikali atakula nyama anayopenda inaendelea kwa sasa lakini ni lazima mipango iwe makini kwa kila timu. Iwe ni kwa timu ambazo zinashiriki Ligi Kuu Bara,…

Read More

LUKAKU AOMBA RADHI CHELSEA

STAA wa Klabu ya Chelsea inayoshiriki Ligi Kuu England, Romelu Lukaku amejitokeza hadharani na kuomba radhi kwa mashabiki wa timu hiyo pamoja na kocha wake. Nyota huyo hivi karibuni alitibua hali ya hewa kwa kuwa aliweka wazi kwamba hafurahishiwa na maisha ndani ya timu hiyo na hakuwa na furaha kabisa. Lukaku alizua taharuki alipokuwa akifanya…

Read More

ARSENAL V LIVERPOOL YAAHIRISHWA

MCHEZO wa nusu fainali ya Carabao Cup kati ya Arsenal na Liverpool uliopangwa kuchezwa leo Alhamis Januari 6 umeahirishwa kutokana na kuongezeka kwa wimbi la UVIKO-19. Mchezo huo ulipangwa kuchezwa Uwanja wa Emirates ambapo baada ya kuahirishwa utapangiwa siku nyingine. Liverpool ilipeleka maombi yao kwa FA kutaka mchezo huo uahirishwe kutokana na wachezaji wake wengi…

Read More

YANGA YATUPIA MABAO 2-0 MBELE YA TAIFA JANG’OMBE

KATIKA michezo wa kwanza leo Yanga wameweza kuibuka na ushindj wa mabao 2-0 mbele ya Taifa Jang’ombe. Mabao ya Yanga yametupiwa na Heritier Makambo dakika ya 32 na lile la pili limepachikwa na Dennis Nkane. Ni bao la kwanza kwa Nkane baada ya kuibuka hapo akitokea kikosi cha Biashara United na amefunga bao hilo dakika…

Read More

YANGA 1-0 TAIFA JANG’OMBE, DAKIKA 45

MABINGWA watetezi wa Kombe la Mapinduzi Yanga wanakwenda mapumziko wakiwa mbele kwa bao moja kwa nunge. Dakika 45 zimekamilika na ubao unasoma Yanga 1-0 Taifa Jang’ombe. Bao la kuongoza limefungwa na Heritier Makambo dakika ya ya 32 akiwa nje ya 18. Pia nyota mpya wa Yanga Dennis Nkane ameanza kikosi cha kwanza leo Januari 5,2022…

Read More

YANGA YAINGIA MKATABA NA KAMPUNI YA KILINET NA N-CARDS

KLABU ya Yanga leo Januari 5  imeingia makubaliano na Kampuni za KILINET na N-Cards kwa ajili ya kutengeneza kadi za kidigitali zitazokuwa zinatumiwa na Wanachama wa timu hiyo. Hiyo ni sehemu ya hatua za awali kwenye mfumo mpya wa uendeshaji ambapo kadi moja itauzwa shilingi 29,000. Kaimu Mtendaji Mkuu wa Yanga, Senzo Mbatha amesema kuwa…

Read More