YANGA YATUPIA MABAO 2-0 MBELE YA TAIFA JANG’OMBE

KATIKA michezo wa kwanza leo Yanga wameweza kuibuka na ushindj wa mabao 2-0 mbele ya Taifa Jang’ombe.

Mabao ya Yanga yametupiwa na Heritier Makambo dakika ya 32 na lile la pili limepachikwa na Dennis Nkane.

Ni bao la kwanza kwa Nkane baada ya kuibuka hapo akitokea kikosi cha Biashara United na amefunga bao hilo dakika ya 50.

Baada ya mchezo Nkane amesema kuwa kwake ni furaha kuona timu inashinda.

“Napenda kuona kwamba timu inashinda na kila mmoja anafurahi namna ambavyo tumeshinda bado kazi inaendelea na makengo yetu ni kufanya vizuri zaidi,”