SIMBA KUMSHUSHA MSHAMBULIAJI HUYU WA KAZI

IMEELEZWA kuwa Sh 800Mil alizoweka Rais wa Heshima wa Simba, Mohamed Dewji ‘Mo’ kwa ajili ya usajili, zimeanza na mshambuliaji wa Orlando Pirates ya Afrika Kusini, Kwame Peprah, raia wa Ghana. Simba imekuwa kwenye mazungumzo ya muda mrefu na Mghana huyo ambaye inaelezwa mkataba wake unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu. Timu hiyo imepanga kukiimarisha…

Read More

UWANJA WA AMAAN:TANZANIA 0-0 CAMEROON

LEO Juni 5,2022 timu ya Taifa ya Wanawake chini ya miaka 17 inacheza mchezo wa marudio kuweza kuwania kufuzu Kombe la Sunia. Mchezo wa kwanza uliochezwa ugenini, U 17 ya Tanzania ilishinda kwa mabao 4-1 hivyo leo wanakamilisha dk 90 za mchezo wa pili. Dakika 45 za kipindi cha kwanza zimekamilika na imekuwa Tanzania U…

Read More

POGBA KUVUTA MKWANJA MREFU UNITED

IMEFICHUKA kuwa Paul Pogba ataondoka na bonasi ya pauni milioni 3.78 (Sh bilioni 11) atakapoachana na Manchester United mara baada ya mkataba wake kufikia tamati mwishoni mwa mwezi huu. United ilithibitisha kuwa kiungo huyo Mfaransa ataondoka Old Trafford mkataba wake utakapomalizika Juni 30, huku pia ikithibitishwa kuwa Jese Lingard naye anasepa. Licha ya kuwa na…

Read More

STARS YAREJEA KUANZA KUIPIGIA HESABU ALGERIA

BAADA ya kupata pointi moja ugenini Jana Juni 4,2022 leo Timu ya Taifa ya Tanzania,Taifa Stars, imewasili Dar kupitia Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere wakitokea Cotonou, Benin walipokuwa kwenye mchezo wa Kundi F kufuzu AFCON. Kwenye mchezo huo dhidi ya Niger ulimalizika kwa sare ya kufungana bao 1-1 na kuwafanya Stars kupata pointi moja….

Read More

SIMBA:TUTASAJILI WACHEZAJI WENYE NJAA YA MAFANIKIO

MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi Simba,Salim Abdallah amesema kuwa msimu ujao watafanya usajili mkubwa kwa kuleta wachezaji wenye njaa ya mafanikio. Kwa sasa Simba ipo kwenye mchakato wa kumsaka kocha mpya baada ya Mei 31,2022 kumchimbisha Pablo Franco ambeya alikuwa kwenye benchi la ufundi. Mchezo wake wa mwisho kukaa benchi ilikuwa Mei 28 mbele ya…

Read More

ANTONIO RUDIGER ASANI MIAKA MINNE REAL MADRID

REAL Madrid imempa dili la miaka minne beki wa kazi akitokea Klabu ya Chelsea ambayo alikuwa akiitumikia. Ni Antonio Rudiger amejiunga bure na Mabingwa wa Ligi ya Ulaya ambao waliinyoosha kwa bao 1-0 Liverpool. Nyota huyo ni raia wa Ujerumani amemaliza mkataba wake ndani ya Stamford Bridge na hakuwa tayari kuweza kuongeza dili jipya zaidi…

Read More

JUVENTUS YAMVUTIA KASI POGBA

KIUNGO mshambuliaji wa Manchester UnitedPaul Pogba inatajwa kwamba anaweza kujiunga na Juventus ambayo imemuwekea mkwanja mrefu kupata saini yake. Nyota huyo mkataba wake unatarajiwa kumeguka ndani ya Manchester United mwisho wa msimu huu na hana mpango wa kuongeza dili jipya kwa kuwa tayari ameshawaaga maosi wake. Alijiunga na United akitokea Klabu ya Juventus na ametoa…

Read More

SIMBA YABAINISHA SABABU ZA KUMCHIMBISHA PABLO

MABOSI Simba  wameweka wazi kwamba kushindwa kutimiza yale aliyosaini kwenye mkataba ni sababu iliyofanya kufutwa kazi kwa Pablo Franco aliyekuwa Kocha Mkuu wa Simba. Mei 31,Simba kupitia kwa Mtendaji Mkuu, Barbara Gonzalez waliweka wazi kwamba wamefikia makubaliano ya kuachana na Pablo kwenye nafasi hiyo na timu kwa sasa ipo chini ya Seleman Matola ambaye ni…

Read More

KAMBOLE AINGIA ANGA ZA YANGA

 IMEELEZWA kuwa Lazarous Kambole anayekipiga ndani ya Klabu ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini yupo kwenye hesabu za  mabosi wa Yanga. Huyo ni mshambuliaji wa kimataifa ambaye anatajwa kuwa kwenye hesabu za vinara hao wa ligi ambao wapo kwenye kusubiri hesabu zikamilike watwae taji la Ligi Kuu Bara kwa kuwa wamewaacha wapinzani wao Simba kwa…

Read More

SHIME:CAMEROON WAGUMU,LAKINI TUTASHINDA

 BAKARI Shime, Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa za Wanawake Tanzania,amesema kuwa mchezo wa marudiano baina yao dhidi ya Timu ya Taifa ya Wasichana wa U 17 Serengeti Girls dhidi ya Cameroon kuwania Kufuzu Kombe la Dunia hautakuwa rahisi. Licha ya kutambua kwamba mchezo huo hautakuwa rahisi kutokana na kila timu kuhitaji ushindi, Shime amebainisha…

Read More

MWENDO WA BIASHARA UNITED NA MBEYA KWANZA UNA JAMBO LAO

KAZI haiwezi kuwa nyepesi kwa kuwa lazima mapambano yawe makubwa katika kufanya hilo jambo ambalo unalihitaji kwa wakati. Kila mmoja kwenye Ligi Kuu Bara kwa sasa anapambana kuweza kufikia malengo ambayo alianza nayo mwanzo wa msimu wa 2021/22 ambao unakaribia kugota mwisho. Hakika ni moja ya msimu wenye ushindani mkubwa na kila timu inafanya vizuri…

Read More

TAIFA STARS KUVAA NIGER LEO

KIM Poulsen, Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania amesema kuwa wapo tayari kwa ajili ya mchezo wa leo wa kuwania kufuzu AFCON 2023. Jana Mei 3,2022 wachezaji wa Timu ya Taifa,Taifa Stars, walifanya mazoezi ya mwisho Stadium L’amitié General Matthieu KEREKOU, Cotonou, Benin kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa Kundi F kufuzu…

Read More