KIMATAIFA MUHIMU KUANZA MAANDALIZI KWA SASA

MUDA uliopo kwa sasa ni mwendelezo wa mashindano yaliyopo mbele kitaifa na kimataifa. Ambacho kinatakiwa ni maandalizi mazuri kwa timu zote. Kila mmoja anapenda kuona matokeo yanapatika kwenye mechi zote. Iwe ni zile za kirafiki ama za ushindani muhimu ushindi kwa kuwa hapo furaha imejificha. Ni muda wa wachezaji kufanya kazi zao kwa umakini bila…

Read More

KUBEBA MATOKEO MFUKONI KUTAWAPOTEZA KIMATAIFA

KILA timu imeshatambua mpinzani wake kwenye  Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kupangwa. Kila timu imetambua ni wapinzani wa aina gani ambao itakabiliana nao kwenye mechi za kimataifa. Kufika kwenye hatua hiyo ni muhimu kuwapa pongezi wahusika kwa kuwa walipambana kufikia malengo. Yanga na Simba kazi kubwa walifanya katika kupata matokeo. Kwa yaliyotokea mpaka kuwa…

Read More

HUU HAPA MTAMBO WA MABAO NDAI YA AZAM FC

KIUNGO mwenye kazi kubwa ndani ya Azam C kutengeneza mipango ya kusaka pointi tatu anaitwa Feisal Salum, Fei Toto. Ni mtambo wa mabao ndani ya kikosi hicho tupo naye kwenye mwendo wa data namna hii:- Mabao yake Mabao matatu dhidi ya Tabora United mchezo uliochezwa Uwanja wa Azam Complex Katika mchezo huo Fei Toto alipachika…

Read More

SERIKALI IAMUE MOJA TU, IZIBEBE MOJA KWA MOJA GHARAMA

KUNA kila sababu ya kusema Serikali ya Jamhuri ya Tanzania chini ya Dk Samia Suluhu Hassan inajitahidi kuonyesha inafanya jambo katika michezo nchini. Inawezekana kwa awamu kadhaa zilizopita, Serikali imekuwa ikishiriki katika michezo katika nyanja mbalimbali. Kipindi hiki kumekuwa na mabadiliko zaidi na mengi yanahusisha hamasa na kidogo usaidizi katika gharama ya timu zetu za…

Read More

HAWAAMINI MACHO YAO SIMBA KIMATAIFA

HAWAAMINI macho yao Power Dynamos wapinzani wa Simba kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kushuhudia wakipokwa tonge mdomoni la kutinga hatua ya makundi. Kwenye mchezo uliochezwa Uwanja wa Azam Complex, Power Dynamos walianza kuwatungua Simba ndani ya dakika 20 za mwanzo kipindi cha pili mambo yalibadilika na kuruhusu nyavu zao kutikishwa. Dakika 90 zilikamilika…

Read More

KUVUNJIKA KWA KOLEO SI MWISHO WA UHUNZI

KWENYE anga la kimataifa tumeona namna ambavyo wawakilishi wa Tanzania walikuwa wakipambana kutafuta matokeo. Mwisho dakika 90 zimeamua nani atakuwa nani. Kwa Yanga walikuwa na faida ya ushindi wa mabao mawili waliyopata ugenini dhidi ya Al Merrikh na Simba wao sare ya mabao 2-2 waliyopata ugenini. Ni wazi kuwa wachezaji wa Yanga walijituma mechi zote…

Read More

WAMOROCCO WANAWASHANGAA WACHEZAJI WA TANZANIA

WACHEZAJI wengi waliopo Tanzania wamekuwa na kiwango kikubwa cha uchezaji lakini hawakuwahi kupitia katika shule za soka maarufu kama Academy. Ili mtoto awe bora ni lazima aanze kulelewa tokea akiwa mdogo akipata mafunzo ya mchezo husika ambao yeye anataka kuutumikia hapo baadaye. Watoto wengi wa Ulaya wamepata bahati kubwa ya kuwa na vyuo bora vya…

Read More

KIMATAIFA MALIZIENI MKIA KWA UMAKINI

WIKI ya kutambua mbivu na mbichi kwenye anga la kimataifa hii hapa imefika ambapo kila mmoja atavuna kile ambacho atakipanda ndani ya dakika 90. Yale majigambo ya nje ya uwanja muda wake unakwenda kugota mwisho kwani ipo wazi kuwa hakuna marefu yasiyokuwa nan cha. Muda huu uliobaki kwa wawakilishi wetu kimataifa ni kuchanga karata kwa…

Read More

KOCHA AL MERRIKH: YANGA INAOGOPESHA

KOCHA wa Al Merrikh, Osamah Nabieh amekiri kwa kusema kuwa Yanga ni moja kati ya timu ambayo inahofiwa kwa sasa barani Afrika kulingana na kile ambacho inakionyesha ndani ya uwanja haswa kutokana na kupata matokeo mazuri na kucheza mpira mzuri. Kocha huyo anayokumbukumbu ya kupokea kichapo cha mabao 2-0 wakiwa nyumbani katika mchezo wa kwanza…

Read More

TUSIJUMUISHE USHABIKI KWENYE MASUALA YA KUUMIZWA KWA INONGA

WAKATI mwingine si vibaya kusema mashabiki wa mpira na hasa Tanzania wamekuwa na mambo mengi sana yanayopaswa kulaaniwa. Binafsi nayaona ni masuala ambayo yanaonyesha ushabiki kupindukia wakati mwingine unakuwa ni tatizo kubwa sana. Ushabiki wa aina hiyo umewafanya mashabiki wengi washindwe kujitambua na ndio maana umeona baadhi ya mashabiki au wahamasishaji wanaotangaza zaidi chuki wamekuwa…

Read More

BALEKE KWENYE KIVULI CHAKE NDANI YA SIMBA

MGANDAMIZO wakati mwingine hutoa kitu halisi na muda mwingine huwa kinakuwa na mvurugano kutokana na aina ya mwanga ambao utakuwa unahusika. Kwenye Ligi Kuu Bara ndani ya Simba kuna mshamuliaji aliyefunga mzunguko wa pili 2022/23 kwa kasi kisha kaanza kuishi kwenye kivuli chake msimu wa 2023/24. Hapa kwenye mwendo wa data tupo na nyota Jean…

Read More

WABABE KAZINI NA REKODI ZAO MATATA HIZI HAPA

MSAKO wa pointi tatu kwenye Ligi Kuu Bara unazidi kupamba moto huku kila timu zikionyesha uimara wake katika kutumia makosa ya wapinzani. Septemba 21 itabaki kwenye rekodi kwa wababe wanne kuwa kazi kusaka ushindi na mwisho wawili wakawapoteza wapinzani wao. Hapa tunakuletea namka kazi ilivyokuwa namna hii:- Mabao ya mapema Mashabiki wa Simba walishuhudia bao…

Read More

KIMATAIFA KAZI BADO HAIJAGOTA MWISHO

TUMEONA namna ambavyo wawakilishi wetu kwenye anga la kimataifa wakiendelea kupambania kombe kufikia malengo ambayo yapo na kila mmoja akiwa anahitaji kuona ushindi unapatikana. Kila timu inaona namna ambavyo kazi inafanyika kutokana na msako wa ushindi kwenye mchezo husika. Ipo hivyo mashindano ya kimataifa hayana mwenyewe ila atakayefanya maandalizi mazuri ni njia nyepesi kupata matokeo….

Read More

AFYA YA WACHEZAJI NI MUHIMU, WACHEZAJI LINDANENI

KAZI kubwa kwenye Ligi Kuu Bara imezidi kuonekana ambapo wachezaji wameonekana wakifanya kweli kwenye kutimiza majukumu yao. Hili ni muhimu kuendelea kwenye kila mchezo jambo ambalo litaongeza umakini kwenye msako wa pointi tatu. Tunaona namna ambavyo kila timu inapambana kutimiza majukumu yake. Kwa wachezaji jukumu lenu ambalo mmepewa ni kutafuta ushindi na suala la kuumizana…

Read More

SIMBA NA YANGA KIMATAIFA, NCHI IPO KAZINI

MAPIGO ya moyo kwenda kasi katika kiwango chake hiyo ni afya, ikitokea kukawa kuna jambo la tofauti limetokea kwa wengi tutasema nchi ipo kazini. Mastaa wa Yanga na Simba leo wana kazi kubwa kusaka ushindi kwenye anga la kimataifa ambapo Watanzania watakuwa wanasubira kuona kitakachovunwa baada ya dakika 90. Ni leo Jumamosi saa 10 jioni,…

Read More