KILICHOMUWEKA NJE AJIBU CHATAJWA

NYOTA wa kikosi cha Azam FC, Ibrahim Ajibu ameweza kurejea katika kikosi hicho hivyo anatarajiwa kuwa miongoni mwa wale watakaoonyesha makeke kwa mechi zijazo. Ingizo hilo jipya ndani ya Azam FC msimu huu liliibuka hapo kutokea ndani ya Simba na halijawa kwenye mwendo mzuri. Sababu kubwa za kukosekana kwenye kikosi hicho ni matatizo ya kifamilia…

Read More

WINGA HUYU WA KAZI AWEKWA RADA ZA YANGA

IMEELEZWA kuwa mabosi wa Yanga wanamtazama kwa ukaribu kiungo wa ASEC Mimosas ya Ivory Coast, Aziz Ki ili waweze kupata saini yake. Nyota huyo pia anatajwa kuingia kwenye rada za Simba ambao nao pia wanahitaji kumpata kwa ajili ya msimu mpya. Nyota huyo ni raia wa Burkina Faso aliweza kufanya vizuri akiwa na timu yake…

Read More

SIMBA KUMCHOMOA KIUNGO KUTOKA KWA WAARABU

IMEELEZWA kuwa miongoni mwa nyota ambao wapo kwenye hesabu za kuweza kusajiliwa ndani ya Simba ni pamoja na kiungo Luis Miquissone. Nyota huyo alikuwa ndani ya Simba msimu wa 2020/21 na alijiunga na Al Ahly msimu wa 2021/22 ambapo kwa sasa bado yupo huku nchini Misri. Waarabu hao wa Misri msimu huu wamekwama kushinda taji…

Read More

RASHFORD AIGOMEA SPURS

 MSHAMBULIAJI wa Manchester United, Marcus Rashford ameigomea ofa ya Tottenham Spurs na badala yake anataka kuanza upya kuipambania namba ndani ya United. Nyota huyo anataka kuanza kupambana upya msimu ujao chini ya Kocha Mkuu, Eric Ten Hag kwa mujibu wa taarifa. Rashford mwenye miaka 24 alikuwa na msimu mbaya ndani ya Old Trafford kwa kuwa…

Read More

LACAZETTE NI MALI YA LYON

MSHAMBULIAJI wa Arsenal Alexandre Lacazette amesajiliwa tena Lyon kwa uhamisho wa bila malipo miaka mitano baada ya kuondoka na kujiunga na The Gunners kwa rekodi ya klabu wakati huo ya euro 46.5m. Lacazette anarejea katika klabu hiyo ya Ufaransa kwa mkataba wa miaka mitatu hadi Juni 2025. Mshambuliaji huyo wa Ufaransa alifunga mabao 54 katika…

Read More

INJINIA AREJESHA FOMU YA KUGOMBEA URAIS

JUNI 9,2022, Injinia Hersi Said amerejesha fomu yake ya kugombea Urais wa Yanga kupitia wawakilishi wake. Injinia amewakilishwa na wazee wa Yanga pamoja na Fredrick Mwakalebela ambaye rasmi amesema kuwa yeye hatogombea na kuwaaga wana Yanga kwenye nafasi yake ya Makamu Mwenyekiti. Mkurugenzi wa uwekezaji wa GSM, Injini Hersi jana alichukuliwa fomu ya kugombea Urais…

Read More

NBC YATAMBULISHA KOMBE JIPYA LA LIGI KUU BARA

 MTENDAJI Mkuu wa Bodi ya Ligi Almas Kasongo ametambulisha Kombe Jipya atakalopewa Bingwa wa Ligi Kuu ya NBC msimu huu wa 2021/2022. Akiongea wakati wa uzinduzi huo Kasongo amewashukuru wanahabari na wadau wote wa mpira kwa michango yao katika kukuza soka la nchi hii, lakini pia namna ambavyo wanauongelea mpira wa nchi pamoja na changamoto…

Read More

MAKOCHA 100 WAOMBA KAZI SIMBA

INATAJWA kwamba makocha zaidi ya 100 wametuma CV zao kwa ajili ya kuoma dili la kuifundisha Klabu ya Simba. Simba kwa sasa ipo chini ya Kaimu Kocha, Seleman Matola ambaye anafanya kazi ya kusimamia mipango ya timu hiyo. Alikuwa ni Pablo Franco ambaye amefutwa kazi Mei 31 kutokana na kushindwa kutimiza malengo ya Simba. Habari…

Read More

BANDA AINGIA ANGA ZA YANGA

 UONGOZI wa Yanga baada ya kuona uwezekano mdogo wa kumpata mshambuliaji Moses Phiri, sasa umehamia kwa mshambuliaji Ricky Banda mwenye uraia wa Zambia anayekipiga Red Arrows. Hapo awali Yanga ilikuwa ikihusishwa kwa karibu katika usajili wa mshambuliaji wa Zesco, Moses Phiri ambaye kwa sasa ni wazi ana asilimia kubwa ya kujiunga na Simba. Katika suala…

Read More

SADIO MANE APANDIWA DAU TENA NA BAYERN MUNICH

BAYERN Munich wanajiandaa kuwasilisha ofa kwa ajili ya kumpata winga Sadio Mane ambaye anakipiga ndani ya Liverpool inayoshiriki Ligi Kuu England. Ni zaidi ya pauni milioni 30 zimetengwa na Bayern Munich kwa ajili ya kumpata mchezaji huyo raia wa Senegal ambaye anahitaji kuondoka hapo. Dau la kwanza lilikuwa pauni milioni 30 mabosi wa Liverpool waliligomea…

Read More

ZLATAN BADO YUYUPO AC MILAN

NYOTA wa Klabu ya AC Milan,Zlatan Ibrahimovic anatarajiwa kuendelea kutumika ndani ya kikosi hicho kwa msimu mwingine tena kwa mujibu wa taarifa. Nyota huyo mwenye miaka 40 alifanyiwa upasuaji wa goti Mei 25 mwaka huu na anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa muda wa miezi sita. Staa huyo msimu wa 2021/22 licha ya majeraha ya…

Read More

NAMNA CAF WALIVYOWEKA ZUIO KOCHA MPYA SIMBA

IMEELEZWA kuwa Rais wa Heshima ya Klabu ya Simba, Mohammed Dewji ‘Mo’ amezuia mipango ya kumleta Kocha Mkuu wa APR ya nchini Rwanda, Mohammed Adil Erradi kutokana kutokidhi vigezo vya Shirikisho la Soka Afrika (CAF). Erradi ni kati ya makocha waliokuwa wakipewa nafasi kubwa ya kuja kuchukua nafasi ya Mhispania, Pablo Franco aliyesitishiwa mkataba wa…

Read More

BIASHARA UNITED YAPATA KOCHA MPYA

UONGOZI wa Biashara United umetangaza benchi jipya la ufundi kwa ajili ya kumaliza mechi nne za msimu 2021/22.  Ni Vivier Bahati ambaye alikuwa kocha mkuu, msaidizi wake Daddy Gilbert na meneja Frank Wabale hawa wote wamefutwa kazi. Kocha Mkuu ni Khalid Adam atakuwa kocha Mkuu wa Biashara United ambayo inapambana kushuka daraja kwa sasa. Kwa…

Read More

TANZANIA YAPOTEZA MBELE YA ALGERIA

TIMU ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars inayonolewa na Kocha Mkuu,Kim Poulsen leo Juni 8,2022  imeambulia kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa Timu ya Taifa ya Algeria katika mechi ya pili ya kufuzu kushiriki fainali za mataifa ya Afrika AFCON zinazotarajiwa kufanyika 2023 nchini Ivory Coast. Ndani ya dk 40 Stars iliweza kujilinda lakini makosa…

Read More