UONGOZI wa Yanga umeweka wazi kuwa kuelekea Wiki ya Mwananchi,Agosti 6,2022 kila kitu Byuti Byuti kama ilivyo slogan yao kwa mwaka huu.
Makamu wa Rais Young Africans SC na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Wiki ya Mwananchi,Arafat Haji amesema kuwa maandalizi yapo vizuri na kila kitu kinakwenda sawa.
“Agosti 6 ndiyo siku pekee ambayo wana Yanga wataona Makombe yote ambayo tumebeba msimu ulioisha kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, pia msimu ujao tutaanza tulipoishia kwa sababu tumefanya sajili bora za kuongeza mafanikio katika kikosi chetu.
“Kila kitu ni Byuti Byuti kuelekea wiki ya Mwananchi kutakuwa na burudani ya kutosha kutoka kwa wasanii mbalimbali pia mtaona vitu byuti uwanjani kutoka kwa wachezaji wetu, Yanga hatuokoti tunasajili ma MVP,” amesema.