SIMBA QUEENS YAIPIGA YANGA 4G

SIMBA Queens imeibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Yanga Princess katika mchezo wa Ligi ya Wanawake. Mchezo huo umechezwa leo Januari 8, Uwanja wa Mkapa na Simba Queens imesepa na pointi zote tatu. Mchezo ujao utakuwa ni wa mzunguko wa pili na unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mo Simba Arena.

Read More

NYOTA BARCELONA ASAINI ASTON VILLA

KIUNGO mshambuliaji wa FC Barcelona, Phillipe Coutinho amejiunga kwa mkopo kwenye klabu ya Aston Villa hii baada ya Villa kudhibitisha kupitia mitandao yake ya kijamii juu makubaliano ya timu zote mbili juu ya sahihi ya Mbrazili huyo.   Coutinho anarejea tena nchini Uingereza baada ya kuondoka kwenye majira ya joto mwaka 2018 alipojiunga na miamba ya Uhispania,…

Read More

NI YANGA V AZAM, SIMBA V NAMUNGO, KOMBE LA MAPINDUZI

KITU pekee ambacho mashabiki wa Simba na Yanga wanakifurahia kwa sasa ni kuziona timu hizo zikiendelea kukipiga kwenye Kombe la Mapinduzi licha ya kubanwa kwenye mechi zao za mwisho za makundi. Vigogo hao wa soka bara licha ya kuwa na sehemu kubwa ya vikosi vyao lakini walishindwa kuzibeba pointi tatu kwenye mechi hizo za mwisho ambapo waliambulia pointi moja tu. Yanga ndiyo walikuwa wa kwanza kucheza ambapo walitoshana…

Read More

YANGA WAPANIA KUVUNJA REKODI KWA SIMBA

KOCHA Mkuu wa Yanga Princess, Edna Lema ‘Morinyo’ ameweka wazi kuwa anataka kufuta uteja mbele ya Simba Queens kwa kushinda kwenye mechi yao ya dabi itakayopigwa leo Jumamosi Januari 8 2022 katika Uwanja wa Mkapa, Dar. Kocha huyo alitoa kauli hiyo wakati wa mkutano kati ya timu hizo na Waandishi wa Habari uliofanyika jana Ijumaa katika Ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF). Edna amesema: “Sina matokeo mazuri au Yanga Princess haina matokeo mazuri mbele ya Simba, ila huu ni mchezo na matokeo ni baada ya…

Read More

SIMBA YAGAWANA POINTI NA MLANDEGE

SIMBA leo Januari 7,2022 imetoshana nguvu bila kufungana na Mlandege FC kwenye mchezo wa pili wa Kombe la Mapinduzi. Dakika 90 zimekamilika kwa ubao wa Uwanja wa Amaan kusoma Simba 0-0 Mlandenge FC. Licha ya Simba kuanza na wachezaji wake wa kikosi cha kwanza ikiwa ni pamoja na kipa namba moja Aishi Manula, mshambuliaji wao…

Read More

MILANGO MIGUMU DAKIKA 45,SIMBA 0-0 MLANDEGE FC

MILANGO ni migumu Uwanja wa Amaan baada ya dakika 45 kumeguka huku ubao ukisoma Simba 0-0 Mlandege FC. Ni mchezo wa Kombe la Mapinduzi ambapo timu hizi zinasaka nafasi ya kutinga hatua ya nusu fainali. Jitihada za Simba kuweza kupata bao la kuongoza ndani ya dakika 45 zimegonga mwamba kutokana na nafasi ambazo wamezitengeneza kushindwa…

Read More

DAKIKA 45, YANGA 1-0 KMKM

UWANJA wa Amaan ni mapumziko Kombe la Mapinduzi baada ya dakika 45 kukamilika. Ubao unasoma Yanga 1-0 KMKM na mtupiaji ni Heritier Makambo kwa pasi ya Dikson Ambundo dakika ya 45. KMKM wamekuwa wakipambana ndani ya dakika 45 lakini wamekwama kutumia nafasi ambazo wamezipata mbele ya Yanga.   Yanga unakwenda mapumziko ikiwa na faida ya…

Read More

SALUM MAYANGA KOCHA MPYA MTIBWA SUGAR

RASMI Salum Mayanga atakuwa kwenye benchi la ufundi la Mtibwa Sugar baada ya kutambulishwa leo Januari 7,2022. Mayanga alikuwa akiinoa timu ya Tanzania Prisons ambapo alikuwa kwenye mwendo mzuri jambo lililowafanya Mtibwa Sugar kuhitaji huduma yake. Anachukua mikoba ya Joseph Omong ambaye alichimbishwa Desemba 14,2021. Kwenye msimamo Mtibwa Sugar ipo nafasi ya 13 ikiwa na…

Read More