YANGA YAKWEA PIPA KUWAFUATA MBEYA KWANZA

KIKOSI cha Yanga kinachonolewa na Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi leo Novemba 28 kimekwea pipa kwa ajili ya kuelekea Mbeya. Ni Air Tanzania itawafikisha Mbeya kwa ajili ya kuweza kuanza kufanya maandalizi ya mwisho baada ya jana Novemba 27 kufanya mmazoezi kwa mara ya mwisho kambini Kigamboni kabla ya leo kusepa. Mchezo wao wa ligi unatarajiwa…

Read More

BANGALA AANDALIWA KWA AJILI YA SIMBA

YANGA imedhamiria kuwafunga kwa mara pili watani wao Simba, ni baada ya kumpumzisha kwa makusudi kiungo wao mkabaji, Mkongomani Yannick Bangala katika mchezo ujao wa Ligi Kuu Bara.   Mchezo ujao wa ligi wa Yanga watacheza dhidi ya Mbeya Kwanza kwenye Uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya ambao Bangala atakuwepo jukwaani akiutazama mchezo huo.   Dabi hiyo inatarajiwa kupigwa Desemba 11, mwaka huu kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam katika mchezo uliopita wa Ngao ya Jamii uliozikutanisha timu hizo, Yanga ilifanikiwa kuwafunga Simba bao 1-0…

Read More

DOZI HII WAMEANDALIWA WAZAMBIA WA SIMBA

KOCHA Mkuu wa Simba, Pablo Franco, raia wa Hispania, amefichua malengo yao makubwa kwa sasa ni kuhakikisha wanawaondoa wapinzani wao katika Kombe la Shirikisho Afrika, Red Arrows ya Zambia kutokana na maandalizi makubwa wanayoyafanya kwa sasa. Simba inatarajia kucheza na Red Arrows ya Zambia katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika kesho Jumapili kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar. Pablo ametoa kauli hiyo kuelekea mchezo wa kwanza wa…

Read More

YACOUBA KUKOSEKANA YANGA MSIMU MZIMA

LICHA ya mafanikio makubwa ya upasuaji wa goti aliofanyiwa kiungo Mburkinabe wa Yanga, Yacouba Songne, imeelezwa kuwa kiungo huyo yupo hatarini kukosa michezo iliyosalia ya msimu huu kutokana na kuuguza jeraha hilo. Yacouba alipata majeraha hayo ya goti kwenye mchezo dhidi ya Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam, ambapo upasuaji wake ulifanyika Novemba 11, mwaka huu. Yacouba tayari amerejea nchini…

Read More

MABOSI SIMBA WAMUWEKEA MTEGO PABLO

WAKATI kesho Pablo Franco akiwa na kibarua cha kusaka ushindi mbele ya Red Arrows katika mchezo wa kimataifa wa Kombe la Shirikisho, mabosi wa Simba wamempa mtego kocha wao kwa kumpa malengo makubwa ambayo anapaswa kuyafikia. Pablo amerithi mikoba ya Didier Gomes ambaye aliomba kuondoka baada ya timu hiyo kuboronga katika Ligi ya Mabingwa Afrika…

Read More

SIMBA YAIPIGIA MATIZI RED ARROWS KWA MKAPA

PABLO Franco, leo Novemba 26 ameongoza mazoezi kwa mara ya kwanza kwa kikosi chake katika Uwanja wa Mkapa. Mazoezi ya leo ni kwa ajili ya mchezo wa Kombe la Shirikisho ambao ni wa mtoano na unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa. Itakuwa ni Novemba 28 ambapo mashabiki 35,000 wa Simba wameruhusiwa kuingia kushuhudia mchezo huo. Kwa…

Read More

RED ARROWS WAPINZANI WA SIMBA WANA MCHECHETO

WAPINZANI wa Simba katika Kombe la Shirikisho barani Afrika, Klabu ya Red Arrows imeweka wazi kuwa nia yao ya kusonga mbele katika michuano hiyo huku wakitamba kufanya vizuri wakiwa ugenini. Red Arrows kutoka Zambia Jumapili Novemba 28 watacheza mchezo wao wa kwanza wa mtoano wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Simba kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar. Mchezo wa marudiano unatarajiwa kufanyika Desemba Mosi nchini Zambia ambapo Simba watakuwa ugenini…

Read More

MASHABIKI RUKSA MECHI YA SIMBA V RED ARROWS KWA MKAPA

MASHABIKI 35,000 ni ruksa kuushuhudia mchezo wa Kombe la Shirikisho ambao unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa, Novemba 28. Kwa mujibu wa Shirikisho la Soka Afrika, (CAF) ni mashabiki hao wataruhusiwa kuwa ndani ya uwanja kushuhudia mchezo huo. Na pia mashabiki hao wanapaswa kufuata taratibu na kanuni za kujilinda dhidi ya Corona. Unatarajiwa kuwa mchezo mkali…

Read More

MOLOKO NDANI YA YANGA AHUSIKA KATIKA MABAO MAWILI

JESUS Moloko ndani ya Yanga kwa msimu wa 2021/22 amehusika katika mabao mawili kati ya mabao 10 ambayo yamefungwa. Ametupia mabao mawili katika ligi akitumiq pasi ya mshambuliaji wa Yanga, Yacouba Songne raia wa Burkina Faso. Kwa sasa Yacouba yupo nje ya uwanja akipata matibabu zaidi baada ya kupata majeraha alipokuwa akitumikia timu hiyo kwenye…

Read More