Serengeti Boys Kucheza Fainali ya Historia Dhidi ya Senegal
TIMU ya Taifa ya Tanzania ya vijana chini ya miaka 17, Serengeti Boys, itashuka dimbani kesho Jumanne Juni 2, 2026 usiku kumenyana na Senegal katika fainali ya michuano ya TotalEnergies CAF U-17 AFCON Morocco 2026 itakayochezwa mjini Rabat, Morocco. Mchezo huo wa fainali unatarajiwa kuchezwa katika Uwanja wa Moulay El Hassan kuanzia saa 4:00 usiku…