KIUNGO mgumu wa Simba Sadio Kanoute atakosekana kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Wydad Casablanca unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa Desemba 19. Nyota huyo katika mechi tatu mfululizo alionyeshwa kadi za njano hivyo atakuwa jukwaani kuwashuhudia wachezaji wenzake wakipambania pointi tatu.