>

YANGA YASEPA NA POINTI TATU ZA GEITA

YANGA imeibuka na ushindi kwenye mchezo wake wa ligi dhidi ya Geita Gold ikiwa ni mzunguko wa pili. Ubao wa Uwanja wa Azam Complex umesoma Yanga 3-1 Geita Gold. Ni Geita Gold wao walianza kupachika bao la kuongoza mapema kipindi cha kwanza dakika ya 19 kupitia kwa Elias Maguli ambalo lilidumu mpaka muda wa mapumziko….

Read More

MTIBWA YAKWAMA KWA SIMBA

MTIBWA Sugar kwa msimu wa 2022/23 imekwama kusepa na ushindi dhidi ya Simba kwenye mechi ambazo wamekutana ndani ya ligi. Katika mzunguko wa kwanza walipokutana Uwanja wa Mkapa, timu hiyo ilpoteza mchezo huo. Baada ya dakika 90 ubao wa Uwanja wa Mkapa ulisoma Simba 5-0 Mtibwa Sugar. Hivyo mzunguko wa kwanza waliacha pointi tatu Uwanja…

Read More

MANCHESTER UNITED YAGAWANA POINTI

WAKIWA Uwanja wa Old Trafford wamegawana pointi mojamoja na timu inayoshikilia mkia. Ubao umesoma Manchester United 0-0 Southampton kwenye msako wa pointi tatu. United waliyeyusha dakika 90 wakiwa pungufu baada ya nyota wao Casemiro kuonyeshwa kadi nyekundu dakika ya 34. Sasa United inafikisha pointi 50 nafasi ya tatu huku Southampton ikiwa nafasi ya 20 na…

Read More

YANGA 0-1 GEITA GOLD

UBAO wa Uwanja wa Azam Complex unasoma Yanga 0-1 Geita Gold ikiwa ni dakika 45 za mwanzo. Bao pekee la uongozi kwa Geita Gold limefungwa na Elias Maguli ambaye ametumia makosa ya safu ya ulinzi ya Yanga. Ni dakika ya 19 Maguli amemtungua kipa namba moja wa Yanga Djigui Diarra. Moja ya mchezo wenye ushindani…

Read More

IHEFU KAMILI KUIKABILI AZAM FC

KOCHA wa Ihefu Temy Felix amesema kuwa wanatambua mchezo wa kesho dhidi ya Azam FC utakuwa mgumu lakini wanahitaji matokeo mazuri. Katika mchezo wa mzunguko wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Azam Complex ubao ulisoma Azam FC 1-0 Ihefu na kuwafanya wayeyushe pointi tatu. “Mchezo muhimu kwetu na tunatambua utakuwa na upinzani mkubwa mashabiki wajitokeze kwa…

Read More

MAYELE KAMILI KUIKABILI GEITA GOLD

FISTON Mayele mshambuliaji wa Yanga amesema kuwa wapo tayari kwa ajili ya mchezo wa kesho dhidi ya Geita Gold. Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Azam Complex saa 1:00 usiku. Ngoma inatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na timu zote kusaka pointi tatu. Mayele amesema:”Ni mchezo muhimu kwetu na tunahitaji kupata pointi tatu mashabiki wawe…

Read More

MTIBWA SUGAR 0-3 SIMBA

DAKIKA 45 za mwanzo zimekamilika Uwanja wa Manungu kwa timu zote kuvuja jasho kusaka mabao ya kuongoza. Mtibwa Sugar 0-3 Simba unasoma ubao wa Uwanja wa Manungu kwa sasa huku mashabiki wakiwa wamejitokeza kwa wingi. Ni Jean Baleke mshambuliaji wa Simba katupia mabao yote matatu hivyo anajihakikishia nafasi ya kusepa na mpira wake. Huu ni…

Read More

AZAM FC WANAIVUTIA KASI IHEFU

KIKOSI cha Azam FC kinatarajiwa kumenyana na Ihefu kwenye mchezo wao ujao wa Ligi Kuu Bara. Azam FC chini ya Kocha Mkuu, Kali Ongala tayari wameanza maandalizi kwa ajili ya mchezo huo. Miongoni mwa wachezaji ambao wameanza maandalizi ni pamoja na Idris Mbombo, Prince Dube, Ayoub Lyanga. Ongala amesema wapo tayari kwa ajili ya mchezo…

Read More

SIMBA INAAMINI ITAPATA UGUMU KWA MTIBWA

JUMA Mgunda, kocha msaidizi wa Simba amesema kuwa wanatambua watapata upinzani mkubwa kwenye mchezo wao dhidi ya Mtibwa Sugar. Simba itakuwa Uwanja wa Manungu kusaka pointi tatu dhidi ya Mtibwa Sugar ambao nao wanazihitaji pia. Kwenye mchezo wa mzunguko wa kwanza ubao wa Uwanja wa Mkapa ulisoma Simba 5-0 Mtibwa Sugar. Mgunda amesema:”Tunategemea kupata ushindani…

Read More