NGUVU IWE KUBWA MAANDALIZI KOMBE LA DUNIA

TAYARI mambo yameshakuwa hadharani kwa wawakilishi wetu kimataifa kwa upande wa Wanawake katika Kombe la Dunia. Hatua ya kwanza waliweza kuipiga ilikuwa ni kuweza kufuzu na kushiriki Kombe la Dunia kwa timu ya Wanawake ya Tanzania, U 17, Serengeti Girls katika hilo kila Mtanzania alitoa pongezi. Kwa sasa ni muda wao wa kuweza kuanza kujipanga…

Read More

WAKATI MWINGINE KUPIGA HESABU KIMATAIFA

WAKATI mwingine tena wa kukamilisha hesabu kwenye mipango ya kimataifa hasa kwa timu ambazo zinakibarua cha kufanya hivyo kimataifa. Haikuwa kazi ngumu kwa msimu uliopita kwa timu za Tanzania kuweza kupeta kimataifa kwa kuwa kila timu ilikuwa inakwenda kwa mwendo wake wa kusuasua. Azam FC licha ya kuwa imara kwenye miundombinu pamoja na wachezaji wazuri…

Read More

MASHINE YA MABAO SIMBA KUPEWA MKONO WA KWA HERI

MEDDIE Kagere mshambuliaji wa mabao ndani ya Simba anatajwa kuwa miongoni mwa mastaa ambao watapigwa chini ndani ya kikosi hicho kinachoshiriki ligi. Simba leo ina kibarua cha kusaka ushindi mbele ya Tanzania Prisons mchezo unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Sokoine. Habari kutoka ndani ya Simba zimeeleza kuwa tayari mabosi wa Simba wameanza mpango wa kusaka mbadala…

Read More

TETESI: MMILIKI MPYA CHELSEA AKUTANA NA WAKALA WA RONALDO

Mmiliki mpya wa Klabu ya Chelsea, Todd Boehly amekutana na Jorge Mendes ambaye ni Wakala wa Cristiano Ronaldo ikidaiwa wamezungumza kuhusu usajili wa Mshambuliaji huyo raia wa Ureno Inaelezwa walikutana wiki iliyopita na mazungmzo yanaendelea. Mkataba wa Ronaldo ndani ya United umebaki mwaka mmoja, klabu hiyo ina nia ya kuendelea naye lakini kumekuwa na taarifa…

Read More

FT:MBEYA CITY 1-1 YANGA, UWANJA WA SOKOINE

MCHEZO wa Ligi Kuu Bara kati ya Mbeya City dhidi ya Yanga umekamilika Uwanja wa Sokoine kwa timu zote mbili kugawana pointi mojamoja. Ni Yanga walianza kupata bao la kuongoza kwenye mchezo wa leo uliokuwa na ushindani mkuwa mwanzo mwisho. Bao la Heritier Makambo ilikuwa dk ya 39 liliweza kujazwa kimiani na lilidumu mpaka dk…

Read More

KOMBE LIPO UWANJA WA SOKOINE,MBEYA CITY 0-1 YANGA

 KOMBE Jipya la Ligi Kuu Bara la NBC lipo Uwanja wa Sokoine, Mbeya,ambapo mabingwa wa msimu wa 2021/22 watakabidhiwa mara baada ya kukamilisha dk 90 mbele ya Mbeya City. Kwa sasa mchezo ni mapumziko ampabo ubao unasoma Mbeya City 0-1 Yanga mtupiaji akiwa ni Heritier Makambo dk ya 39 kwa shuti lililoweza kugonga mwaba kabla…

Read More

WAPE TABASAMU KUFANYIKA UWANJA WA SABASABA,MORO

ANAANDIKA Dickson Job,beki wa kikosi cha Yanga na timu ya Taifa ya Tanzania,Taifa Starsnamna hii:-Habari watanzania. Mimi ni DICKSON JOB mchezaji wa Klabu ya Yanga. Nawakaribisha kutuunga mkono Katika siku maalumu tuliyoiandaa kwaajili ya kutoa Shukran zetu kwa jamii tuliyoipa jina la WAPE TABASAMU itakayofanyika tarehe 08/07/2022 Mkoani Morogoro. Siku hii ni maalumu kwaajili ya…

Read More

KLOPP BADO ANAMKUMBUKA MANE

JURGEN Klopp, Kocha Mkuu wa Liverpool anaamini kwamba kuondoka kwa Sadio Mane ni jamo gumu kwake kwenda nalo sawa kwa sasa.  Mane raia wa Senegal sasa atakuwa ni mali ya Bayern Munich baada ya timu hiyo kukamilisha usajili wake. Unakuwa ni usajili wa tatu kwa Bayern Munich kukamilika ambapo Mane anakwenda kuchukua mikoba ya Robert…

Read More

RATIBA YA LIGI KUU BARA IPO HIVI

LEO Juni 25 Ligi Kuu Tanzania Bara inaendelea ambapo ratiba yake ni moto kwa timu zinazopambana kushuka daraja kwa kuwa hatma yao itaanza kufahamika leo. Ni Yanga ambao ni mabingwa wa ligi wao hawana presha zaidi ya kuendelea kusaka rekodi za kutofungwa kwa msimu wa 2021/22 ndani ya ligi Muziki kamili leo utakuwa namna hii:-Coastal…

Read More

YANGA KUIKABILI MBEYA CITY

KIKOSI cha Yanga kinachonolewa na Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi leo kitakuwa na kibarua cha kusaka ushindi mbele ya Mbeya City kwenye mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa. Jana wachezaji wa Yanga ikiwa ni pamoja na Zawad Mauya, Fiston Mayele,Feisal Salum walikuwa ni miongoni mwa nyota ambao walifanya mazoezi ya mwisho kwenye Uwanja wa Sokoine Mbeya…

Read More

GEITA GOLD YAFUNGIWA NA FIFA KUSAJILI

SHIRIKISHO la Kimataifa la Soka (FIFA) limeifungia Klabu ya Geita Gold kusajili wachezaji hadi itakapomlipa aliyekuwa kocha wa timu hiyo Ettiene Ndayiragije. Kocha huyo raia wa Burundi alifungua madai dhidi ya Geita Gold akidai fidia ya kuvunjiwa mkataba pamoja na malipo mengine wakati akiifundisha timu hiyo ya mkoani Geita. Kwa mujibu wa taratibu za FIFA,…

Read More