MANCHESTER UNITED YA ONANA HAIJAONANA
WIKI ya 10 ndani ya Premier League, Manchester United wamechapwa kwenye Dabi na kupoteza pointi tatu dhidi ya Manchester City. Nyumbani walikuwa Uwanja wa Old Trafford walishuhudia ubao ukisoma Manchester United 0-3 Manchester City. Mwamba Erling Haaland alitupia mabao mawili dakika ya 26 na 49 huku Phil Foden akitupia bao moja usiku dakika ya 80….