Home International HII HAPA ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA USHAURI SIMBA

HII HAPA ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA USHAURI SIMBA

AMEANDIKA Mohammed Dewji, (Mo) Rais wa heshima wa Simba:-

Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita tangu tuanze safari ya Mabadililko Klabu yetu imepiga hatua kubwa sana katika nyanja mbali mbali.

Pamoja na maendeleo ambayo Klabu yetu imepiga katika kipindi hiki cha miaka mitano lakini malengo yetu bado hatujayafikia.

Mojawapo ya majukumu yangu kama Raisi wa heshima wa Simba ni kuhakikisha Uongozi na Utawala bora unazidi kuboreshwa kila wakati ili kuzidi kusukuma gurudumu la maendeleo ya Klabu yetu.

Hivyo basi baada ya kushauriana na Mwenyekiti wa Bodi na Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, nimewateua wafuatao kuwa Wajumbe wa Baraza la Ushauri ( Advisory Board) la Klabu ya Simba.

1. Jaji Thomas Mihayo Mwenyekiti

2. Hassan Dalali-Mjumbe

3. Ismail Aden Rage-Mjumbe

4. Evans Aveva-Mjumbe

5. Faroukh Baghoza – Mjumbe

6. Swedi Nkwabi-Mjumbe

7. Azim Dewji-Mjumbe

8. Kassim Dewji-Mjumbe

9. Musleh Al-Ruweh-Mjumbe

10. Mohamed Nassor-Mjumbe

11. Mulamu Ng’ambi-Mjumbe

12. Octavian Mshiu-Mjumbe

13. Prof Janabi-Mjumbe

14. Hassan Kipusi-Mjumbe

15. Geofrey Nyange-Mjumbe

16. Gerald Yambi-Mjumbe

17. Moses Kaluwa-Mjumbe

18.Crescentius Magori-Mjumbe

19. Juma Pinto- Mjumbe

20. Mwina Kaduguda-Mjumbe

21. Idd Kajuna-Mjumbe

Sekretariat ya Simba itaratibu mikutano ya Baraza hili la Ushauri.

Kazi kubwa ya Baraza hili itakuwa ni kuishauri Bodi juu ya maendeleo ya Klabu ya Simba, Uongozi na utawala bora.

Previous articleYANGA DHIDI YA SINGIDA FOUNTAIN GATE KUNA KITU KIZITO
Next articleMUHIMU KUWA NA MAANDALIZI BORA KILA WAKATI