KUMBE YANGA BADO INAJITAFUTA

BAADA ya Yanga kujikusanyia pointi 15 katika michezo mitano ya kwanza ya Ligi Kuu Bara msimu huu, kocha mkuu wa timu hiyo, Nasreddine Nabi amewataka mashabiki wao wasiwe na hofu kwani huu ni mwanzo tu, mazuri zaidi yanakuja.   Yanga imekuwa kwenye kiwango bora msimu huu ambapo imefanikiwa kuweka rekodi ya kushinda mechi tano za mwanzo kwenye Ligi Kuu Bara kitu ambacho timu zingine zimeshindwa kufanya. Akizungumza na Spoti Xtra, Nabi alifichua kwamba, alitumia muda mrefu kuitengeza…

Read More

POULSEN AKUBALI UWEZO WA WACHEZAJI WAKE

KIM Poulsen, Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars amesema kuwa uwezo wa wachezaji ambao wapo kwenye kikosi hicho ni mkubwa na anaamini kwamba watampa matokeo chanya kwenye mechi za kimataifa. Akizungumza na Championi Jumamosi, Poulsen alisema kuwa kila mchezaji ambaye ameuita kikosini alipata muda wa kumfuatilia na kuona uwezo wake na…

Read More

SALAH NI BORA DUNIANI

MSHAMBULIAJI wa zamani wa Liverpool, Fernando Torres amesema kuwa nyota Mohamed Salah ambaye ni mshambuliaj ndiye mchezaji bora kwa sasa duniani.   Salah anawania tuzo ya mchezaji bora wa mwaka ya dunia ambayo itatolewa mwezi ujao na Shirikisho la Soka la Kimataifa,(Fifa) na watu wengi wamekuwa wakiamini kuwa anastahili kutwaa tuzo hiyo. Torres aliweza kuutazama…

Read More

GUARDIOLA AKUBALI MUZIKI WA UNITED

KOCHA wa Manchester City, Pep Guardiola amekubali muziki wa wapinzani wake Manchester United kwa kuweka wazi kuwa ina wachezaji wazuri. Majira ya saa 9:30 muda wa kujipatia msosi Manchester United itakuwa ikimenyana na Manchester City kwenye mchezo wa Ligi Kuu England utakaopigwa Uwanja wa Old Trafford. Unatajwa kuwa moja ya mchezo unaosubiriwa kwa shauku kubwa…

Read More

XAVI KOCHA MPYA BARCELONA

XAVI Hernandez atakuja kuwa kocha mpya wa Barcelona baada ya mabosi wake Al Sadd kuthibitisha kuhusu hilo. Taarifa rasmi ambayo imetolewa na Al Sadd imeeleza kuwa wamefikia makubaliano mazuri na Xavi kuhusu suala la malipo pamoja na kumuacha aende kwa amani kuanza changamoto mpya. Xavi alikuwa anahusishwa kurejea kwa mara nyingine ndani ya Nou Camp…

Read More

CHAMA AKUBALI KUREJEA SIMBA

ALIYEKUWA kiungo wa Simba, Mzambia, Clatous Chama, amebainisha kwamba, yupo tayari kurudi katika kikosi hicho endapo atatakiwa kufanya hivyo.Chama aliyecheza Simba kwa misimu mitatu kuanzia 2018 hadi 2021, msimu huu amejiunga na RS Berkane ya Morocco.   Akiwa Simba, kiungo huyo alipata mafanikio makubwa ikiwemo kuwa mchezaji bora wa Ligi Kuu Bara msimu wa 2019/20 na kiungo bora 2020/21. Simba msimu huu imeanza kwa kasi ya kawaida huku kati ya upungufu ambao umekuwa ukibainishwa ni kukosekana kwa Chama na Luis Miquissone ambao waliondoka mwishoni mwa msimu uliopita.   Akizungumzia uwezekano wa kurudi Simba, Chama…

Read More

UNAI ATAJWA NEWCASTLE UNITED

UNAI Emery, Kocha Mkuu wa Villarreal amewaambia mabosi wa timu hiyo kwamba Klabu ya Newcastle United inaonekana kumuhitaji licha ya kwamba hawajapeleka ofa kwa wakati huu.   Kocha huyo inaelezwa kuwa atachukua nafasi ya aliyekuwa kocha wa Newcastle United, Steve Bruce ambaye alifungashiwa virago kwenye timu hiyo baada ya timu hiyo kupata wawekezaji wapya mwezi…

Read More

RONALDO ANAKIWASHA TU HUKO

CRISTIANO Ronaldo nyota wa Manchester United mbele ya mashabiki 14,443 katika Uwanja wa Gewiss aliibuka kuwa mchezaji bora wa mchezo huo jambo linalomaanisha kwamba hana jambo dogo.   Kwenye sare ya kufungana mabao 2-2 dhidi ya Atalanta, Ronaldo alipachika mabao mawili dakika ya 45 na 90. Mabao ya Atalanta yalipachikwa na Josip Ilicic dakika ya…

Read More

ARGUERO ASHAURIWA KUKAA NJE MIEZI MITATU

MSHAMBULIAJI wa kikosi cha Barcelona, Sergio Arguero  atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa miezi mitatu ikiaminika kuwa ni kutokana na kusumbuliwa na tatizo la moyo.   Nyota huyo ambaye ameibuka ndani ya kikosi hicho kinachoshoshiriki La Liga akitokea Klabu ya Manchester City inayoshiriki Ligi Kuu England alipata tatizo hilo Oktoba 30 wakati timu hiyo…

Read More

CONTE ATAMBULISHWA NDANI YA TOTTENHAM

BREAKING:Antonio Conte amerejea ndani ya Ligi Kuu England na atakuwa ni Kocha Mkuu wa Klabu ya Tottenham Hotspur inayoshiriki ligi hiyo pendwa duniani.   Conte anachukua mikoba ya Nuno Espirito ambaye alichimbishwa katika kikosi hicho jana Novemba kutokana na mwendo mbovu wa timu hiyo kwa kile kilichoelezwa kuwa ameshindwa kufikia malengo ya timu hiyo. Mazungumzo…

Read More

CONTE KUSAINI DILI JIPYA LEO TOTTENHAM

ANTONIO Conte anatarajiwa kusaini dili jipya leo Jumanne ili kuweza kuwa Kocha Mkuu wa Tottenham. Conte anakwenda kuchukua mikoba ya Nuno Espirito ambaye alichimbishwa mazima jana Novemba Mosi. Espirito alifungashiwa virago kutokana na mwendo mbovu wa timu hiyo ambapo kwenye mechi zake sita za Ligi Kuu England alipoteza mechi nne. Kichapo cha mabao 3-0 dhidi…

Read More

BRENDAN HAFIKIRII KUIFUNDISHA MANCHESTER UNITED

BOSI wa Leicester City, Brendan Rodgers amesisitiza kuwa hafikirii kwenda kuifundisha Manchester United. Rodgers amesisitiza kuwa malengo yake ni kuweza kuona timu yake ya sasa inatwaa mataji zaidi. Kocha huyo amekuwa akitajwa kwenda kuinoa Manchester United ambayo inaweza kumtimua Ole Gunnar Solkjaer. Bosi huyo amesema:”Malengo yangu siku zote ni kuona Leicester inaendelea kuwa bora,kutwaa mataji…

Read More

LIVERPOOL YAMPA KOCHA WAKE HASIRA

KOCHA Mkuu wa Liverpool, Jurgen Klopp amegeuka mbogo kwa wachezaji wake kwa kuwaeleza kuwa walicheza chini ya kiwango kwenye mchezo wao wa Ligi Kuu England na kuwafanya watoshane nguvu na wapinzani wao Brighton.   Ilikuwa ni Oktoba 30 ambapo Liverpool walikuwa wanapewa nafasi ya kushinda kwa kuwa walikuwa wametoka kuwanyoosha mabao matano Manchester United ila…

Read More

MESSI MAMBO MAGUMU PSG

NYOTA wa kikosi cha PSG, mshambuliaji Lionel Messi mambo kwake ni magumu kwenye ishu ya kucheka na nyavu baada ya kuweka rekodi ya kucheza mechi tano bila kufunga. Ni giza nene limeendelea kutanda kwenye macho yake kwa sasa staa huyo ambaye alikuwa akikiwasha ndani ya Barcelona kwani tayari amecheza mechi hizo ndani ya Ligue 1…

Read More

HAZARD AWEKWA RADA ZA CHELSEA

NYOTA wa Real Madrid, Eden Hazard ambaye mambo kwake yamekuwa magumu ndani ya kikosi hicho anatajwa kuingia kwenye rada za Newcastle pamoja na Chelsea. Nyota huyo hana furaha ndani ya Real Madrid kutokana na kusumbuliwa na majeraha ya mara kwa mara jambo ambalo limefanya ashindwe kuwa kwenye ubora ambao alikuwa nao alipokuwa akicheza ndani ya…

Read More

OLE BADO YUPO SANA MANCHESTER UNITED

Kocha Mkuu wa Manchester Unite, Ole Gunnar Solskjaer anatarajiwa kubaki na kuendelea kuinoa timu hiyo licha ya mwendelezo wa matokeo mabovu hususani ya bao 5-0 aliyapata juzi baada ya kupigwa na Liverpool, Sky Sports Italia imethibitisha.   Mkurugenzi Mtendaji wa Klabu ya Manchester, Richard Arnold jana alivunja appointment zote za vikao vya wageni ili kukutana na Mmiliki wa Klabu hiyo, Joel…

Read More