SIMBA INANUKIA FEDHA,YANGA MAMBO BYUTI BYUTI
Simba inanukia fedha,Yanga mambo byuti byuti,ndani ya Spoti Xtra Jumanne
Simba inanukia fedha,Yanga mambo byuti byuti,ndani ya Spoti Xtra Jumanne
PARIS Saint Germain,(PSG) wamefanikiwa kufungua msimu wa 2022/23 kwa kutwaa taji la Trophee des Champions ambapo Lionel Mess,Neymar Jr na Sergio Ramos waliweza kufanya kweli. PSG waliibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Nantes kwenye mchezo uliokuwa ni wa ufunguzi wa msimu mpya wa 2022/23. Kwenye mchezo huo mabao ya PSG yalifungwa na Messi…
KLABU ya Arsenal imemtangaza rasmi Martin Odegaard kuwa ni nahodha mpya kuelekea msimu mpya wa 2022/2023. Arsenal ilimsajili mchezaji huyo kutoka timu ya Real Madrid kwa mkopo kabla ya kukamilisha dili la kumsajili moja kwa moja kwa ada ya Paundi milioni 30 kufuatia kufanya vizuri ndani ya kikosi hicho cha washika mtutu wa London. Hivyo…
KIUNGO wa kazi Mudhathir Yahya hatakuwa sehemu ya kikosi cha Azam FC baada ya mkataba wake kuisha na mabosi wake hao kuamua kutomuongezea mkataba mpya. Muda hakuweza kusafiri na timu kuelekea nchini Misri kwa kuwa alikuwa na majukumu kwenye timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars. Stras ilikuwa na kazi ya kusaka tiketi ya kucheza…
UONGOZI wa Yanga umeweka wazi kuwa kuelekea Wiki ya Mwananchi,Agosti 6,2022 kila kitu Byuti Byuti kama ilivyo slogan yao kwa mwaka huu. Makamu wa Rais Young Africans SC na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Wiki ya Mwananchi,Arafat Haji amesema kuwa maandalizi yapo vizuri na kila kitu kinakwenda sawa. “Agosti 6 ndiyo siku pekee ambayo…
AZAM FC bado wanendelea na kambi nchini Misri ambapo kwa sasa wanaendelea na mazoezi kwa ajili ya msimu mpya wa 2022/23,kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Azam FC,Zakaria Thabit ameweka wazi kuwa wamekamilisha masuala ya ICT kwa wachezaji wa kigeni
MTEDAJI Mkuu wa Simba,Barbara Gonzale amesema kuwa leo ni kubwa kwa Simba na kampuni ya kubashiri ya M-Bet ambao ni wadhamini wao wakuu walioweka mkwanja mrefu kwa muda wa miaka mitano. Ni mkataba wenye thamani ya bilioni 26 kwa miaka mitano ikiwa ni mkwanja mrefu watakaopokea Simba kwa mafungumafungu. Barbara amesema:”Leo ni siku kubwa kwa…
WALTER Harson aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa KMC ameweza kuwashukuru maosi wake hao na sasa anakwenda kuanza changamoto mpya ndani ya kikosi cha Yanga. Ujumbe wake ambao amewaandikia mashabiki wake pamoja na KMC unasomeka namna hii:”Imekuwa miaka minne yenye kujifunza na kukua katika tasnia. Nafasi niliyoipata ya kuhudumu kama Mtendaji Mkuu wa Klabu kwa kipindi chote…
USHINDI unaleta furaha,ushindi unaleta kicheko ushindi unarejesha lile tabasamu ambalo lilikuwa limejificha kwenye sura ya yule aliyekuwa na makasiriko. Unadhani ushindi unaleta hayo tu,hapana kuna mengi ambayo yanaletwa na ushindi ikiwa ni pamoja na furaha na kuhisi kwamba kila kitu unachogusa kinakutii na kile ambacho hauna mamlaka nacho kinakusikiliza kwa umakini. Ushindi upi ambao unaweza…
NDANI ya Yanga kwa sasa ni raha na vicheko tu kutokana na fedha ambazo zinaendelea kuingia kwenye timu hiyo kupitia wadhamini ambapo mabosi wa timu hiyo mapema tu wametamba wanataka kubeba mataji yote kama msimu uliopita. Mabosi hao wameongeza kuwa wanataka kubeba mataji yao yote waliyotwaa msimu uliopita ya Ngao ya Jamii, Ligi Kuu na…
SIMBA watamba tunarudi na kasi ya kiberenge,mshtuko Senzo kun’goka Yanga ndani ya Championi Jumatatu
MTENDAJI Mkuu wa Simba Barbara Gonzalez amesema kuwa msimu huu klabu hiyo imejipanga kurudisha makombe yote ya ndani na kuhakikisha inafika nusu fainali ya ligi ya Mabingwa Afrika. Barbara ameyasema hayo kwenye uzinduzi wa Simba Week ulifanyika Mbagala Zakheim Dar es salaam ambapo pia ameongeza kuwa usajili bado unaendelea na kuanzia wiki ijayo wataendelea kushusha…
JUMLA ya timu saba za Maveterans zitashiriki katika bonanza maalum la mpira wa miguu litakalofanyika leo Jumapili (Julai 31, 2022) kwenye Uwanja wa Bora Kijitonyama. Bonanza hilo limeandaliwa na taasisi ya ukaguzi wa mahesabu, ushauri wa kifedha, biashara na masuala ya kodi ya Techno Auditors kwa kushirikiana na timu ya Kijitonyama Veterans. Mkurugenzi Mtendaji wa…
HATIMAYE mshambuliaji wa Yanga, Fiston Mayele amevunja ukimya juu ya mkataba wake na Yanga, ambapo ameweka wazi kuwa yeye si mchezaji wa mkopo bali alisaini mkataba wa miaka miwili na bado amebakiza mwaka mmoja. Mayele alijiunga na Yanga Agosti 1, 2021 kwa mkataba wa miaka miwili akitokea katika Klabu ya AS Vita ya kwao DR…
LIVERPOOL imetwaa taji la Ngao ya Jamii baada ya kuyeyuka kwa miaka 16 bila kutwaa taji hilo. Mara ya mwisho kuweza kutwaa taji hilo ilikuwa ni mwaka 2006 baada ya kushinda mabao 2-1 dhidi ya Chelsea. Usiku wa kuamkia leo Julai 31 imeweza kushinda kwa mabao 3-1 dhidi ya Manchester City. Mshambuliaji mpya wa Liverpool,…
WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa alikuwa mgeni rasmi katika toleo la tatu la NBC Dodoma Marathon. Ilikuwa ni Marathon iliyokuwa na ushindani mkubwa na ilivutia zaidi ya washiriki 4,000 kutoka nchi 8 tofautitofauti ambayo walishiriki. Lengo kuu ni kutafuta fedha za kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi…
ZIMEBAKI siku nane kuweza kufika Agosti 8/2022 ambayo itakuwa ni siku ya Simba Day leo Uongozi wa timu hiyo umeweza kuzindua rasmi Wiki ya Simba katika Viwanja vya Mbagala Zakhiem,Dar. Miongoni wa waliokuwepo kwenye uzinduzi huo ambao umehudhiuriwa na mashabiki wengi wa Simba ni pamoja na Mtendaji Mkuu wa Simba,Barbara Gonzalez. Kwa mujibu wa Meneja…