Home Uncategorized UWANJA WA MKAPA: SIMBA 1-5 YANGA

UWANJA WA MKAPA: SIMBA 1-5 YANGA

Kipindi cha pili Yanga walionyesha wanahitaji ushindi na kufunga mabao kupitia kwa Maxi Nzengeli ambaye alifunga mawili dakika ya 64, 77, Aziz KI dakika ya 73, Pacome bao la tano dakika ya 87 kwa mkwaju wa penalti.

Kariakoo Dabi Uwanja wa Mkapa upinzani ni mkubwa kwa timu zote mbili kusaka ushindi kwenye mchezo huo.

Dakika 45 za mwanzo ubao umesoma Simba 1-1 Yanga.

Bao la Yanga limefungwa dakika ya tatu na Kennedy Musonda na bao la Simba limefungwa na Kibu Dennis dakika ya 8.

Ndani ya kipindi kimoja mabao mawili yamepatikana kwa watani hawa wa jadi wanaosaka pointi tatu.

Previous articleJESHI LA SIMBA DHIDI YA YANGA HILI HAPA
Next articleSIMBA WATOA TAMKO BAADA YA KUPIGWA 5 G NA YANGA