Home International MANE APIGWA FAINI NDEFU KWELI BAYERN

MANE APIGWA FAINI NDEFU KWELI BAYERN

BAADA ya Sadio Mane kumpiga mchezaji mwenzake wa bayern Munich, Leroy Sane wiki iliyopita nyota huyo amepigwa faini ya pauni 250,000, (Sh.724,445,000).

Pia inatajwa kuwa staa huyo raia wa Senegal yupo kwenye hesabu za kuuzwa mwishoni mwa msimu huu.

Mane alimchapa ngumi ya mdomo Sane kwenye chumba cha kubadilishia nguo wiki iliyopita kwa madai kuwa Sane alimkejeli kwa lugha na vitendo vya kibaguzi baada ya mchezo dhidi ya Manchester City.

Sane alionekana akiwa amevimba mdomo wakati Bayern Munich walipoivaa Hoffenheim wikiendi iliyopita na Mane hakuwepo kwenye mchezo huo wa Bundesliga.

Mane amesimamishwa kwa kitendo hicho huku akikatwa mshahara wake wa pauni milioni 17, (sh.49.2) kwa mwaka.

Hii ni faini kubwa kwa Bayern Munich kutolewa katika historia yao.

Previous articleYANGA KUWAFUATA RIVERS UNITED KAMILIKAMILI
Next articleAZAM FC HESABU KWA RUVU SHOOTING