Home International MANCHESTER UNITED YAOMBWA MECHI KUPELEKWA MBELE

MANCHESTER UNITED YAOMBWA MECHI KUPELEKWA MBELE

MANCHESTER, ENGLAND - NOVEMBER 06: Cristiano Ronaldo of Manchester United during the Premier League match between Manchester United and Manchester City at Old Trafford on November 6, 2021 in Manchester, England. (Photo by Daniel Chesterton/Offside/Offside via Getty Images)

KLABU ya Manchester United imeomba Ligi Kuu ya Uingereza kuahirisha mchezo wa leo dhidi ya Brentford baada ya kulazimika kusitisha mazoezi ya kikosi chake cha kwanza Desemba 13 kotokana na Corona.

Kitabu cha mwongozo cha Ligi Kuu ya 2021/22 kinajumuisha itifaki za UVIKO-19, na kinaruhusu bodi ya Ligi Kuu kupanga upya au kuahirisha mechi ya ligi kutokana na sababu za kipekee.

Hatahivyo, kuanzia mechi za leo Jumatano mashabiki wa soka nchini Uingereza watahitajika kuonyesha ushahidi wa kuchanjwa na kutokuwa na maabukizi kuhudhuria mechi yoyote ambapo pia hawapaswi kuzidi mashabiki 10,000.

Vilabu vyote 20 vinavyoshiriki Ligi kuu vimetakiwa kurejea kwenye huduma za dharura ikiwemo kukaa umbali na kuvaa barakoa.

Previous articleMUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA CHAMPIONI JUMATANO
Next articleNYOTA WATANO SIMBA WATAPIGWA PANGA