Home International ATLETICO YAFUZU UEFA, SUAREZ HAAMINI

ATLETICO YAFUZU UEFA, SUAREZ HAAMINI

ATLETICO Madrid imefanikiwa kufuzu kwenda hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Porto huku staa wake Luis Suarez akiwa haamini anachokiona na kumwaga machozi baada ya kuumia na kutolewa uwanjani.

Atletico ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao hayo 3-1 katika mchezo uliochezwa Uwanja wa Do Dragao,Porto.

Suarez alianza kikosi cha kwanza alitolewa dakika ya 13 na akaenda benchi huku akimwaga machozi.

Timu hiyo ilikuwa kundi B la maajabu ambalo lilikuwa na Liverpool, Porto, AC Milan na Atletico wenyewe na zilizofuzu ni Liverpool na Atletico watakwenda 16 bora na Porto wao watakwenda Europa.

Previous articleMUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA SPOTI XTRA JUMANNE
Next articleNABI:MIMI NI MTU WA KAZI SIO MANENOMANENO