Home Uncategorized MERIDIAN GAMING GROUP KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA COVID – 19

MERIDIAN GAMING GROUP KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA COVID – 19

Tangu mwanzo wa janga la COVID-19, kampuni zote za Meridian Gaming Group zimekuwa zikifanya jitihada za makusudi katika kuzisaidia jamii sehemu mbalimbali duniani.

 

Mchango wa kampuni hii katika kupambana na Covid-19 ni mkubwa kama ambavyo Meridian Gaming Group imeonesha kwenye matokeo yake ya mwaka 2021 katika kupambana na janga hili.  Meridian imeripoti kuchangia zaidi ya £1M kwenye miradi na misaada inayohusiana na Covid. Mchango huo umezifikia zaidi ya hospitali na vituo vya afya 350 barani Ulaya, Amerika na Africa.

 

Kwa zaidi ya miezi 18 sasa, Meridian Gaming imeendelea kuzisaidia hospitali za Taifa, vituo vya afya, nyumba salama, mashirika ya ustawi wa jamii na mashirika ya afya yaliyopo Kusini Mashariki mwa Ulaya, Umoja wa Ulaya, Amerika ya Kati, Africa na Asia.

Pia, kampuni [Meridian Gaming Group] imeshirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO) katika kusaidia mpango wake wa Misaada ya COVID-19 duniani. Kupitia mashirikiano haya, WHO imeweza kuzisaidia nchi zilizoathirika zaidi duniani katika kampeni za kupambana na COVID-19.

Kwa upekee wake, Meridian Gaming Group wanashikilia rekodi katika kampeni ya kusaidia kurejesha hali nzuri za kiuchumi na kijamii ambazo ziliathiriwa na janga la COVID-19.

Kama ambavyo magonjwa mengine yanavyoendelea kushika kasi wakati huu wa janga la COVID-19. Kwa miaka mingi, Meridian Group imekuwa ikiyaisaidia mashirika ya kitaifa yanayojihusisha na ustawi wa watoto na wazazi wao katika upatikanaji wa matibabu kwa wakati kwa kupitia michango yao.

 

Jamii zetu zimepatwa na majaribu makubwa ambayo kwa namna moja ama nyingine, hatujawahi kupitia hali kama hii. Kwa sababu hii, Meridian inakuwa ni mfano wa kutukumbusha umuhimu wa dunia kusimama pamoja, jambo hili linapaswa kuwa endelevu katika nyakati za zintofahamu kama hizi.

Meridianbet – Bashiri Popote, Wakati Wowote.

Previous articlePABLO AANZA KAZI SIMBA
Next articlePABLO NA DAKIKA ZAKE 60,NABI ATOA NENO, NDANI YA CHAMPIONI JUMAMOSI