MZAMBIA AITAKA NAMBA YA YACOUBA YANGA
MSHAMBULIAJI wa Zanaco ya Zambia, Moses Phiri ambaye anahusishwa kujiunga na Yanga amesema kuwa anatamani kuona anavaa jezi namba 10 katika timu mpya atayojiunga nayo kutokana na kuamini kuwa ni namba ya bahati kwake. Katika klabu ya Yanga jezi namba 10 imekuwa ikivaliwa na Yacouba Songne ambaye alikabidhiwa jezi hiyo tangu alipowasili akitokea Burkina Faso….