TIMU ya taifa ya Mali anayocheza kipa namba moja wa Yanga, Djigui Diarra iliwafungashia virago wapinzani wao Burkina Faso anayocheza Aziz KI anayecheza Klabu ya Yanga.
Ndani ya dakika 90 kwenye hatua ya 16 bora mshindi aliyetinga robo fainali ya Kombe la mataifa ya Afrika (Afcon) ni Mali baada ya kutinga Burkina Faso mabao 2-1 katika mchezo uliochezwa Uwanja wa Amadou Gon Coulibaly Ivory Coast.
Mabao ya mchezo huo kwa upande wa Mali yamefungwa na Edmond Tapsoba aliyejifunga dakika ya tatu na Lassine Sinayoko dakika ya 47’ huku la Burkina Faso likifungwa na Betrand Traore 57 kwa mkwaju wa penalti akimpoteza mlinda mlango Diarra.
Kwa ushindi huo Mali itakutana na Ivory Coast Februari 3 katika robo fainali inayotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa ndani ya dakika 90.
Tottenham Hotspur forward Dominic Solanke battles with Crystal Palace defender Maxence Lacroix during the English championship Premier League football match between Crystal Palace and Tottenham Hotspur on 27 October 2024 at Selhurst Park in London, England - Photo Ian Stephen / ProSportsImages / DPPI (Photo by IAN STEPHEN / ProSportsImages / DPPI via AFP)