El Clásico Ya Moto: FC Barcelona vs Real Madrid CF Kuamua Bingwa La Liga

Pata shika Leo Mei 9 saa 10:00 usiku Uwanja wa Spotify Camp Nou utakuwa mwenyeji wa mchezo wa El Clasico kati ya Barcelona nafasi ya 1 na Real Madrid nafasi ya 2.

Barcelona wakiongoza Ligi wakiwa na pointi 88, wana pointi 11 mbele ya Real Madrid walio na pointi 77 . Kwa tofauti hiyo, wanahitaji sare au ushindi tu kutwaa taji la ubingwa katika uwanja wao mbele ya Barcelona wapinzani wao wakubwa, tukio ambalo lingekuwa adhimu kwa mashabiki wa nyumbani .

Barcelona wanakosa mshambuliaji wao mahiri Lamine Yamal aliyepata mjeraha hadi mwisho wa msimu, lakini wanamrejesha Raphinha na Jules Kounde ambao wanatarajiwa kuanza .

Upande wa Real Madrid, orodha ya majeruhi ni kubwa ikiwemo Ferland Mendy, Eder Militao, Arda Guler na Rodrygo Goes ambao wamekwishamaliza msimu . Kipa Thibaut Courtois anatarajiwa kurejea, hata hivyo Kylian Mbappe bado ana shaka ya kucheza baada ya jeraha lake la paja, na kumekuwa na taarifa za mvutano ndani ya kikosi cha Madrid kuhusu ucheleweshaji wa uponyaji wake.

Katika michezo mitano ya mwisho ya Ligi Kuu kati ya timu hizi, Barcelona wameshinda mara tatu, wakipoteza mara moja na sare moja . Barcelona wamekuwa wakitawala katika michezo ya hivi karibuni ikiwemo ushindi wa 3-2 kwenye Fainali ya Super Cup mwanzoni mwa mwaka.

Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Uchambuzi wa timu unaonyesha kuwa Barcelona wana mashambulizi yenye usawa kutoka pande zote za uwanja, wakati Real Madrid wanategemea sana ubavu wa kushoto kupitia Vinicius Junior, jambo ambalo limekuwa uwezekano wao .

Kocha Hansi Flick ana tatizo la kuchagua kati ya Frenkie de Jong na Gavi kuwa mwenzi wa Pedri kwenye kiungo cha kati Gavi anatarajiwa kuanza baada ya kucheza mechi bora hivi karibuni huku De Jong akiwa anarejea kutoka jeraha . Mbele, Robert Lewandowski atakuwa mshambuliaji mkuu akisaidiwa na Raphinha upande wa kushoto na mchezaji mwingine kulia badala ya Yamal mwenye jeraha .

Kwa Real Madrid, karibu nafasi zote za ulinzi zimeathirika na majeruhi, na beki mbadala Alvaro Carreras anaweza kuanza upande wa kushoto akishirikiana na Antonio Rudiger . Jude Bellingham na Brahim Diaz wanatarajiwa kuwa wachezaji muhimu.Jisajili