KWA upande wa wachezaji wa Simba viwango vyao kwa sasa ni maji kupwa maji kujaa, mchezaji anaweza kucheza mchezo wa leo vizuri kesho akawa katika kiwango cha chini.
Miongoni mwa wachezaji hao ndani ya Simba ni Willy Onana, ukimtazama aliyecheza mchezo dhidi ya Namungo kisha ukamuona aliyecheza dhidi ya Mtibwa Sugar tofauti kabisa.
Hii ni hali inayowatesa wachezaji wengi wa Simba na benchi la ufundi, mbele ya Mtibwa Sugar nafasi tano za wazi ndani ya 18 alikosa utulivu na maamuzi mazuri katika kuzitumia nafasi.