MASHUJAA FC inayotumia Uwanja wa Lake Tanganyika kwa mechi za nyumbani wamerejea kambini kwa maandalizi ya mechi zijazo ndani ya ligi.
Timu hiyo Mei 31 2026 rasmi ilirejea kambini na kuanza maandalizi kwa mchezo ujao unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Lake Tanganyika.
Mashujaa FC vs Yanga SC ni mchezao ujao kwenye ratiba ambapo utakuwa ni mzunguko wa pili kwa wababe hawa kukutana uwanjani.
Mchezo wa mzunguko wa kwanza Yanga SC ilivuna pointi 3 mazima hivyo itakuwa ni vita ya kusaka rekodi ya mwendelezo wa mzunguko wa kwanza na timu nyingine ikiwa kwenye hesabu kutibua rekodi za mzunguko wa kwanza.
Mashujaa FC kwenye msimamo wa ligi ipo nafasi ya 11 imekusanya pointi 27 inakutana na Yanga SC yenye pointi 60 nafasi ya kwanza kwenye msimamo.
…
Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu. Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.
Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.