>

HIZI HAPA REKODI ZA RAUNDI YA SABA LIGI YA WANAWAKE BONGO

LIGI ya Wanawake Tanzania kazi inaendelea kwa kila timu kuwa kwenye msako wa pointi tatu na kwenye raundi ya saba kuna maajabu saba yameandikwa tunakugusia baadhi namna hii:- Mabao 12 yamefungwa kwenye mzunguko wa saba baada ya mechi tano kuchezwa ikionyesha ugumu wa ligi kuendelea tofauti na ilivyokuwa mzunguko wa sita yalipofungwa mabao 13. Hakuna…

Read More

OKRAH APEWA KIFAA MAALUM YANGA

MADAKTARI wa Yanga wanaangalia uwezekano mkubwa wa kumpa kifaa maalum cha ‘Mask’ kiungo wake mpya Augustine Okrah aliyepata jeraha eneo la puani. Kiungo huyo alipata majeraha hayo katika Kombe la Mapinduzi mwezi Januari, baada ya kugongana na mchezaji wa timu pinzani na kupata majeraha katika mishipa ya puani. Nyota huyo aliyejiunga na Yanga katika dirisha…

Read More

AUCHO NDANI YA NYUMBA DHIDI YA KAGERA

KOCHA Mkuu wa Yanga amechukua maamuzi ya kuwabakisha Jijini Dar es Salaam mabeki wake tegemeo nahodha Bakari Mwamnyeto na Ibrahim Hamad ‘Bacca’ kwa hofu ya kujitonyesha majeraha huku kiungo mkabaji Khalid Aucho akiungana na msafara wa timu hiyo, baada ya kumaliza adhabu ya michezo mitatu. Kikosi cha Yanga jana alfajiri kilipanda Ndege kuelekea Mkoani Kagera…

Read More

SIMBA YAWASILI KIGOMA KUWAKABILI MASHUJAA

LIGI Kuu Tanzania Bara inarejea ambapo timu zote zipo kwenye hesabu za msako wa pointi tatu muhimu. Januari 31 Simba ilifunga kwa mchezo wa Azam Sports Federation dhidi ya Tembo uliochezwa Uwanja wa Azam Complex. Februari Mosi Kikosi cha Simba SC, kimetua mkoani Kigoma kwa ajili ya kukabiliana na Mashujaa FC kwenye mchezo wa ligi…

Read More

KISA INONGA, BENCHIKHA AWACHENJIA MABOSI SIMBA

BENCHI la Ufundi la Simba, ambalo lipo chini ya Kocha Mkuu Mualgeria, Abdelhak Benchikha limezuia mauzo ya beki wao kati Mkongomani, Hennock Inonga. Mkongomani huyo ni kati ya wachezaji wanaounda kikosi cha DR Congo, ambacho kimefuzu hatua ya Robo Fainali ya Kombe la Mataifa Afrika (Afcon) huko nchini Ivory Coast baada ya kuwaondoa Misri katika…

Read More

FOUNTAIN GATE YAIPIGIA HESABU SIMBA QUEENS

TIMU yenye vipaji vikubwa na uwekezaji imara ndani ya Ligi ya Wanawake Tanzania, Fountain Gate Princess inayotumia Uwanja wa Jamhuri, Dodoma kwa mechi za nyumbani inaivutia kasi Simba Queens. Ipo wazi kuwa mchezo wao uliopita wakiwa nyumbani walipoteza kwa kufungwa bao 1-0 dhidi ya JKT Tanzania na kuziacha pointi tatu zikisepa mazima. Mchezo wao unafoata…

Read More

YANGA HAO WAIFUATA KAGERA SUGAR

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Bara, Yanga mapema Februari Mosi wameanza safari kueleka Bukoba kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Kagera Sugar unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Kaitaba Februari 2 2024. Timu hiyo Januari 30 ilikuwa na kibarua cha kusaka ushindi kwenye mchezo wa raundi ya Pili Azam Sports Federation ilikuwa dhidi…

Read More