Home Sports NAMUNGO FC WAPIGA HESABU KUMALIZANA NA DODOMA JIJI

NAMUNGO FC WAPIGA HESABU KUMALIZANA NA DODOMA JIJI

KOCHA Mkuu wa Namungo FC Dennis Kitambi amesema kuwa wanaimani kubwa ya kupata matokeo mazuri kwenye mchezo ujao wa ligi dhidi ya Dodoma Jiji

Timu hiyo ya Namungo mchezo wake uliopita ilishinda mbele ya Azam FC kwa mabao 2-1 mchezo uliochezwa Uwanja wa AzamComplex.

Inatarajiwa kucheza na Dodoma Jiji, Juni 6 Uwanja wa Majaliwa ikiwa ni mzunguko wa pili.

“Tulipata matokeo mazuri mchezo uliopita ugenini hapo tunakwenda kufanya maandalizi kwa ajili ya mchezo wetu dhidi ya Dodoma Jiji ambao hautakuwa mwepesi.

“Kikubwa ni kufanyia kazi makosa kwenye mechi zetu zote kwani licha ya kupata ushindi bado kuna makosa ambayo yamekuwa yakifanyika kwa wachezaji hilo tutalifanyia kazi,”

Namungo imefikisha pointi 39 ikiwa nafasi ya tano kwenye msimamo baada ya kucheza mechi 28.

Kwenye mchezo huo kiungo Shiza Kichuya ni miongoni mwa waliofunga bao Uwanja wa Azam Complex wakiwa ugenini.

Previous articleYANGA WAANIKA MBINU WATAKAZOTUMIA KUWAMALIZA WAARABU
Next articleMANCHESTER UNITED KWENYE HESABU ZA MASON