KOCHA Mkuu wa KMC, Jamhuri Kihwelo, ‘Julio’ ameanza mikwara kwa kubainisha kuwa kinachotazamwa kwenye ligi ni namna ya kumaliza.
Mbele ya Singida Big Stars inayonolewa na Hans Pluijm ilisepa na pointi tatu mazima.
Ikumbukwe kwamba mchezo wake wa pili kukaa benchi akiwa na KMC baada ya kubeba mikoba ya Thiery Hitimana amesepa na pointi tatu.
Ubao wa Uwanja wa Uhuru baada ya dakika 90 Mei 12 ulisoma KMC 2-0 Singida Big Stars.
Mchezo wa kwanza ilikuwa ugenini alishuhudia ubao wa Uwanja wa Jamhuri, Dodoma ukisoma Dodoma Jiji 1-0 KMC.