UONGOZI wa Dodoma Jiji umeweka wazi kuwa baada ya kupoteza mchezo wao wa ligi dhidi ya Mtibwa Sugar hasira zao wanazihamishia kwa Ihefu .
Kwenye mchezo waliokuwa Uwanja wa Manungu walipoteza kwa kufungwa mabao 2-1.
Leo Februari 24,2023 Dodoma Jiji wana kazi ya kusaka pointi tatu muhimu dhidi ya Ihefu ya Mbeya.
Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa saa 1:00 usiku kwa timu hizo uonyeshana ubabe wao.
Ofisa Habari wa Dodoma Jiji, Moses Mpunga amesema kuwa kushindwa kupata matokeo mchezo uliopita hasira zinahamia kwenye mchezo dhidi ya Ihefu.
“Maandalizi yapo vizuri tunamshukuru Mungu na tupo tayari kwa ajili ya kupambana kwenye mchezo huo ili kuweza kupata pointi tatu muhimu.
“Wapinzani wetu tunawaheshimu tutaingia kwa tahadhari kubwa maana kila timu inahitaji matokeo ili kuweze kujiweka kwenye nafasi nzuri kwenye ligi kuu,”.
Kiingilio kwenye mchezo wa leo ni buku tu unawaona mastaa wote wa Ihefu na Dodoma Jiji.