Home International MANCHESTER UNITED WAINYOOSHA BARCELONA

MANCHESTER UNITED WAINYOOSHA BARCELONA

Manchester United wamepindua meza dhidi ya Barcelona na ubao ulisoma Manchester United 2-1 Barcelona.

Ni katika mchezo wa Europa League uliochezwa Uwanja wa Old Trafford.

Robert Lewandowski alianza kupachika bao kwa mkwaju wa penalti dakika ya 18 ngoma iliwekwa Sawa na Fred dakika ya 47.

Msumari wa pili kwa Manchester United ulijazwa kimiani na Antony dakika ya 73.

Manchester United wanasonga mbele kwa jumla ya mabao 4-3 Barcelona katika Europa League.

Previous articleMERIDIANBET YATOA BODABODA NA TV USSD & KASINO YA MTANDAONI
Next articleDODOMA JIJI KUMALIZANA NA IHEFU