Home International MOROCCO YAUSHANGAZA ULIMWENGU

MOROCCO YAUSHANGAZA ULIMWENGU

ULIMWENGU wa mpira umeshuhudia maajabu leo baada ya timu ya taifa ya Morocco kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya timu ya taifa ya Ubegiji.

Ngoma ilikuwa nzito kuamini kwamba Morocco ingeibuka na ushindi kwenye mchezo huo ambao ulikuwa na ushindani mkubwa lakini maajabu ya mpira yamekamilika.

Ni mabao ya Abdelhamid Sabri dakika ya 73 na lile la pili lilipachikwa na Zakaria Aboukhal dakika ya 90+2.

Kwenye kundi F Morocco wanaongoza kundi wakiwa na pointi 4 na Ubelgiji ni nafasi ya pili a pointi tatu.

Pia kwenye mchezo wa leo ni mashuti 10 kila timu ilipiga huku Ubelgiji mashuti manne yakilenga lango na mashuti matatu yakilenga lango kwa Morocco.

Previous articlePOLISI TANZANIA 0-2 SIMBA
Next articleSIMBA YASEPA NA POINTI TATU, MANULA ATUNGULIWA