Home Uncategorized BECKHAM ATAJWA KUINUNUA MAN UNITED

BECKHAM ATAJWA KUINUNUA MAN UNITED

 NYOTA wa zamani wa Manchester United, David Bekham anatajwa kuwa kwenye mpango wa kuinunua klabu.

Staa huyo anatajwa kuwa kwenye mchakato wa kuwa kwenye muunganiko na wawekezaji wengine ili kuongeza nguvu na nafasi ya kushinda dili hilo baada ya familia ya Glazers kutangaza kuiweka sokoni.

The Glazers waliinunua Man United kwa pauni milioni 790 ilikuwa mwaka 2005 wameiweka sokoni kwa sasa timu hiyo.

Ilikuwa ni Jumanne ya wiki hii ampabo gazeti la Mirror Football limeripoti kuwa wamepanga kuiuza kwa pauni bilioni 8.

Kwenye mahojiano na Sky Sports mwezi Mei, Beckham alisema:”Kuna mabadiliko ya kufanywa hakuna timu nyingi ambazo yale ambayo wamepitia katika miaka michache iliyopita,”.

Previous articlePINGA UKATILI WA KIJINSIA KWA WANAWAKE NA MERIDIANBET!
Next articleBANGALA. AZIZ KI TAYARI KUIKABILI MBEYA CITY