Home International TAREHE YA UFUNGUZI KOMBE LA DUNIA YARUDISHWA NYUMA

TAREHE YA UFUNGUZI KOMBE LA DUNIA YARUDISHWA NYUMA

TAREHE ya ufunguzi wa michuano ya Fainali za Kombe la Dunia nchini Qatar imerudiswa nyuma siku moja ili kuruhusu wenyeji kufungua pazia hilo.

Tarehe ya ufunguzi wa mashindano hayo ilipaswa kuwa Novemba 21, 2022 huko Qatar siku ya Jumatatu, kungekuwa na mchezo kati ya Senegal dhidi ya Uholanzi.

Baada ya maombi kutoka kwa wenyeji Qatar Baraza la mashindano hayo limeridhia kurudisha mashindano siku moja nyuma ili wenyeji wafungue pazia hilo Jumapili ya Novemba 20 wakicheza dhidi ya Ecuador.

Previous articleSITA WACHAGULIWA KAMATI YA MASHINDANO YANGA
Next articleRAIS FIFA ASISITIZA USHIRIKIANO KATIKA KILA HATUA