Home International JUVENTUS YAKUBALI KUMUUZA BEKI WAO

JUVENTUS YAKUBALI KUMUUZA BEKI WAO

CASTELLON, SPAIN - FEBRUARY 22: Matthijs de Ligt of Juventus during the UEFA Champions League match between Villarreal v Juventus at the Estadio de la Ceramica on February 22, 2022 in Castellon Spain (Photo by David S. Bustamante/Soccrates/Getty Images)

KLABU ya Juventus ya Italia imekubali kumuuza beki wake wa kati, Matthijs de Ligt (22) kwenda  kwa mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich kwa ada ya Paundi Milioni 68 (Tsh. 186,320,000,000)

Taarifa kutoka Ujerumani zinaeleza kuwa beki huyo wa kimataifa wa Uholanzi atasaini mkataba wa miaka mitano na Bayern mara baada ya kukamilisha vipimo vya afya anavyotarajia kufanya leo katika jiji la Munich.

De Ligt anaondoka Juventus akiwa amekaa kwa misimu mitatu, akicheza mechi 177 na kufunga magoli nane. pia, alishinda taji la Serie A katika msimu wa 2019/20.

Previous articleSAUTI:GEORGE MPOLE NDO BASI TENA
Next articleMALALE HAMSINI YATIMIA BAADA YA MUDA MREFU