BARCELONA wamefikia hatua nzuri ya kuipata saini ya staa wa Bayern Munich, Robert Lewandowski kwa ajili ya kuwa naye kwenye kikosi hicho.
Ni kandarasi ya miaka mitatu wamefikia makubaliano ya kumpa mkataba mshambuliaji huyo.
Wakati wowote kuanzia sasa Klabu ya Barcelona watamtangaza rasmi Lewandowski.
Nyota huyo alikuwa amesaliwa na kandarasi ya mwaka mmoja ndani ya Bayern Munich ambao wameweka wazi kwamba wamefikia makualiano mazuri na Barcelona kwa ajili ya mchezaji huyo kujiunga na timu hiyo.
Staa huyo ni raia wa Poland anatajwa kujiunga na Barcelona kwa euro 45 milioni na itaongezwa nyingine 5 kufanya iwe euro milioni 50 ikumbukwe kuwa alifunga mabao 35 msimu uliopita alipokuwa ni mfungaji bora ndani ya Bundesliga.
Tottenham Hotspur forward Dominic Solanke battles with Crystal Palace defender Maxence Lacroix during the English championship Premier League football match between Crystal Palace and Tottenham Hotspur on 27 October 2024 at Selhurst Park in London, England - Photo Ian Stephen / ProSportsImages / DPPI (Photo by IAN STEPHEN / ProSportsImages / DPPI via AFP)