Home Sports AZIZ KI NI NJANO NA KIJANI

AZIZ KI NI NJANO NA KIJANI

MUDA wowote kuanzia sasa huenda Yanga ikamtambulisha nyota wao mpya ambaye ni Aziz KI ambaye anacheza ndani ya kikosi cha ASEC Mimosas.

Yanga inaendelea kufanya usajili kwa ajili ya maboresho ya kikosi hicho ambacho kitashiriki Ligi ya Mabingwa Afrika.

Yanga watawapa kile ambacho mashabiki wao wanasubiri utambulisho wa staa huyo raia wa Ivory Coast.

Nyota wengine ambao wametambulishwa Yanga ni pamoja na Bernard Morrison, Gael Bigirimana, Lazarous Kambole na Joyce Lomalisa.

Ofisa Habari wa Yanga,Haji Manara ameweka wazi kwamba wanahitaji kufanya usajili makini na mzuri.

Previous articleKIUNGO MPYA ATAMBULISHWA SIMBA RAIA WA GHANA
Next articleKAZI IMEANZA,MAYELE AJA NA STAILI MPYA