VIDEO:MASTAA YANGA WALEJEA DAR,SIMBA WAWAPOKEA

MASTAA wa Yanga ambao walikuwa wanashiriki Kombe la Mapinduzi pamoja na viongozi leo Januari 11 wamerejea Dar wakitokeza Zanzibar ambapo walikuwa na kazi ya kutetea Kombe la Mapinudzi ila walivuliwa na Azam FC baada ya kupoteza kwenye changamoto ya penalti.

Baada ya dakika 90 kwenye mchezo huo ubao wa Uwanja wa Amaan ulisoma Azam FC 0-0 Yanga na kwenye penalti ilikuwa Azam FC 9-8 Yanga hivyo Azam FC wamebaki Zanzibar wanakibarua cha kusaka ushindi mbele ya Simba, Januari 13.