DAKIKA 45, YANGA 1-0 KMKM

UWANJA wa Amaan ni mapumziko Kombe la Mapinduzi baada ya dakika 45 kukamilika.

Ubao unasoma Yanga 1-0 KMKM na mtupiaji ni Heritier Makambo kwa pasi ya Dikson Ambundo dakika ya 45.

KMKM wamekuwa wakipambana ndani ya dakika 45 lakini wamekwama kutumia nafasi ambazo wamezipata mbele ya Yanga.

 

Yanga unakwenda mapumziko ikiwa na faida ya bao moja ambalo linawapa hali ya kujiamini katika kulinda ama kuongeza ushindi lakini ni mpaka dakika 45 za kipindi cha pili zitaamua.