YANGA WATOA TAMKO KUHUSU KAULI ZA BOSI SIMBA

UONGOZI wa Klabu ya Yanga umetoa taarifa ya kusikitishwa na kauli iliyotolewa na Mwenyekiti wa wanachama wa klabu ya Simba, Ndg Murtaza Mangungu baada ya mchezo wa jana kati ya Simba na Yanga.

Murtaza Mangungu aliwashutumu TFF na Bodi ya Ligi kuwa waliwaruhusu viongozi wa Yanga kuingia eneo la VVIP bila kadi huku Mkurugenzi Mkuu wa Simba akizuiwa.

Mwenyekiti pia alitoa shutuma kuwa TFF wana dhumuni la kuipa ubingwa klabu ya Yanga