HAALAND, MAN CITY BADO KIDOGO TU

MTENDAJI Mkuu wa Borussia Dortmund, Sebastian Kehl, amefunguka kuwa dili na hatma ya Erling Haaland itajulikana wiki ijayo. Haaland amekuwa akihusishwa kujiunga na timu tofauti za Ulaya, ingawa Manchester City ikionekana kuwa katika nafasi nzuri ya kumsajili. Staa huyo amekuwa kwenye kiwango bora tangu atue Dortmund, Januari 2020 akitokea RB Salzburg ya Austria.  Mwezi uliopita…

Read More

BECKHAM AMZUIA RONALDO KUONDOKA UNITED

STAA mkongwe wa soka, David Beckham amesema anatamani kuona staa wa Manchester United, Cristiano Ronaldo anasalia kikosini hapo kwani ni mchezaji muhimu. Hii ni baada ya kuwepo tetesi kuwa huenda Ronaldo akatimka kikosini hapo, baada ya Man United kushindwa kufuzu kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao, licha ya kuwa na mkataba wa mwaka mmoja…

Read More

STRAIKA WA MABAO AKUBALI KUSAINI YANGA

BAADA ya tetesi nyingi kuzagaa kuhusishwa kusaini mkataba Yanga, mshambuliaji wa Geita Gold, George Mpole ametoa sharti moja kubwa kwa timu hiyo. Mpole ni kati ya wachezaji wanaohusishwa kutua Yanga kuelekea msimu ujao ambapo timu hiyo ina uhakika wa kushiriki michuano ya kimataifa inayosimamiwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF). Mshambuliaji huyo hivi sasa yupo…

Read More

KAGERA SUGAR YATUMA UJUMBE HUU SIMBA

BUBERWA Birikes, Kocha Msaidizi wa Kagera Sugar amesema kuwa watafanya kazi kubwa kupata ushindi mbele ya Simba kesho kwenye mchezo wa ligi. Kesho Mei 11, Kagera Sugar ina kazi ya kusaka pointi tatu mbele ya Simba kwenye mchezo unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa. Akizungumza na Saleh Jembe,Birikes amesema kuwa wanatambua mchezo wao dhidi ya Simba…

Read More

SPORTPESA YAKABIDHI MILIONI 50

HATIMAYE Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Michezo ya Kubashiri ya SportPesa Tanzania, Tarimba Abbas, amemkabidhi Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Simba, Barbara Gonzalez, hundi ya Shilingi milioni 50 kama bonansi baada ya kufanikiwa kuingia katika hatua ya Robo Fainali ya Michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika. Makabidhiano hayo yamefanyika Makao Makuu…

Read More

YANGA:BADO TUTAPAMBANA KUPATA MATOKEO

HAJI Manara, Ofisa Habari wa Yanga amesema kuwa bado wana nafasi ya kufanya vizuri kwenye mechi zijazo za ligi. Manara amesema kuwa kushindwa kupata matokeo kwenye mechi zilizopita haina maana kwamba hawatakuwa imara Yanga ni vinara wa ligi wanawania kutwaa Kombe la Ligi la 28 kwa kuwa wanayo 27 mpaka muda huu. Jana walilazimisha sare…

Read More

YANGA YAKWAMA MBELE YA TANZANIA PRISONS

VINARA wa Ligi Kuu Bara, Yanga chini ya Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi wamekwama kusepa na pointi tatu mbele ya Tanzania Prisons kwenye mchezo uliokuwa na ushindani mkubwa. Hata Prisons nao wamekwama kupata pointi tatu zaidi ya kuambulia pointi moja wakiwa kwenye hatari ya kushuka daraja. Kwenye msimamo Prisons ipo nafasi ya 14 na pointi 23…

Read More

SIMBA YASIMULIA MATESO YA DAKIKA 270

SELEMAN Matola,Kocha Msaidizi wa Simba amesema kuwa wamekuwa kwenye mwendo usiofurahisha kwenye mechi tatu mfululizo jambo wanalolifanyia kazi. Kwenye mechi hizo tatu za ligi ambazo ni dakika 270 katika msako wa pointi 9 waliambulia pointi tatu pekee na kuacha mazima pointi 6 ambazo ni mateso kwao huku wakifungwa mabao mawili sawa na yale ambayo walifunga….

Read More

SIMBA BADO HAIJAKATIA TAMAA UBINGWA

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba wameweka wazi kwamba bado hawajakata tamaa kuhusu kuweza kutetea taji lao hilo kwa msimu huu. Jana,Mei 8, Simba iliweza kupata ushindi wa mabao 4-1 mbele ya Ruvu Shooting huku nahodha John Bocco akiwa ni miongoni mwa watupiaji akifunga bao lake la kwanza msimu wa 2021/22 kwenye ligi….

Read More

NABI:TUTASHINDA MBELE YA PRISONS

NASREDDINE Nabi, Kocha Mkuu wa Yanaga amesema kuwa kuelekea mchezo wao wa ligi dhidi ya Tanzania Prisons wanaamini kwamba watashinda. Leo Mei 9, vinara hao wa ligi wanatarajia kusaka pointi tatu mbele ya Prisons ambao nao wanahitaji pointi hizo, Uwanja wa Mkapa. Maandalizi ya mwisho ameweka wazi kwamba yamekamilika na miongoni mwa wachezaji ambao walikuwa…

Read More

KMC WAIVUTIA KASI MTIBWA SUGAR

KIKOSI cha KMC FC leo Mei 9 kimeanza mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa ligi dhidi ya Mtibwa Sugar utakaopigwa Alhamisi ya Mei 12 katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam. Timu hiyo ya Manispaa ya Kinondoni chini ya Kocha Mkuu, Thierry Hitimana inajiandaa na mchezo huo muhimu ikiwa nyumbani na hivyo…

Read More

MAYELE AWAKIMBIZA TANZANIA PRISONS

WAKATI leo kikosi cha Tanzania Prisons ikiwa na kazi ya kuikabili Yanga,safu yake ya ushambuliaji inaonekana kuwa pasua kichwa kwenye utupiaji. Ikiwa imecheza jumla ya mechi 22 ni mabao 15 imeweza kufunga ndani ya ligi katika dakika 1,980 ikiwa na wastani wa kufunga bao moja kila baada ya dk 132. Kinara wa utupiaji wa mabao…

Read More

KICHUYA APELEKWA YANGA

WAKATI ikitajwa kwamba mabosi wa Simba wanalijadili jina la Shiza Ramadhan Kichuya kwenye usajili wao msimu ujao, baba mzazi wa kiungo huyo, Ramadhan Kichuya amebainisha kwamba, anataka kumuona kijana wake akijiunga na Yanga SC. Baba Kichuya amesema mwanawe huyo atakuwa na wakati mzuri zaidi akiichezea Yanga na siyo Simba ambayo amekuwa na mapenzi nayo kwa…

Read More