ARTETA AKASIRISHWA KUTOLEWA KOMBE LA FA

MIKEL Arteta, Kocha Mkuu wa Arsenal amesema kuwa ni maumivu makubwa wameyapata baada ya kupoteza mbele ya Nottm Forest na kutolewa kwenye Kombe la FA. Katika mchezo wa raundi ya tatu ya Kombe la FA ubao wa Uwanja wa City Ground ulisoma Nottm Forest 1-0 Arsenal. Bao pekee la ushindi lilifungwa na Lewis Grabban dakika…

Read More

VAR KUTUMIKA AFCON, MAMBO YANAANZA LEO

HATIMAYE kwa mara ya kwanza katika historia ya michuano ya AFCON, mechi zote 52 zitatumia marefa wasaidizi wa picha za video (Video Assistant Referees – VAR) huko Cameroon. Michuano hiyo itaanza rasmi leo Jumapili Januari 9, 2022 ambapo wenyeji Cameroon watacheza na Burkinafaso katika uwanja wa Olembe huko Yaounde. Mechi ya mwisho itachezwa Februari 6…

Read More

RALF AKIRI NYOTA MAN U WANATAKA KUSEPA

RALF Rangnick, Kocha Mkuu wa Manchester United kwa muda amekiri kwamba mastaa kadhaa wa timu hiyo wanataka kuondoka mara tu baada ya mikataba yao kuisha. Hivi karibuni ilielezwa kuwa mastaa 17 wa kikosi cha Manchester United inayoshiriki Ligi Kuu England wanataka kuondoka kutokana na kuona mambo hayaendi ndani ya timu hiyo. Kocha huyo hajaweka wazi…

Read More

NYOTA BARCELONA ASAINI ASTON VILLA

KIUNGO mshambuliaji wa FC Barcelona, Phillipe Coutinho amejiunga kwa mkopo kwenye klabu ya Aston Villa hii baada ya Villa kudhibitisha kupitia mitandao yake ya kijamii juu makubaliano ya timu zote mbili juu ya sahihi ya Mbrazili huyo.   Coutinho anarejea tena nchini Uingereza baada ya kuondoka kwenye majira ya joto mwaka 2018 alipojiunga na miamba ya Uhispania,…

Read More

MASTAA MANCHESTER UNITED 17 WANATAKA KUSEPA

MANCHESTER United ipo katika wakati mgumu hasa kutokana na kudaiwa kuwa kuna wimbi kubwa la wachezaji wanataka kuondoka wakati huu wa Januari au mwishoni mwa msimu huu.   Kwa ufupi ni kuwa kuna hali tete ndani ya Old Trafford, ambapo inaelezwa kuwa kuna wachezaji takribani 17 ambao wanaweza kuondoka.   Morali ndani ya klabu hiyo…

Read More

LUKAKU AOMBA RADHI CHELSEA

STAA wa Klabu ya Chelsea inayoshiriki Ligi Kuu England, Romelu Lukaku amejitokeza hadharani na kuomba radhi kwa mashabiki wa timu hiyo pamoja na kocha wake. Nyota huyo hivi karibuni alitibua hali ya hewa kwa kuwa aliweka wazi kwamba hafurahishiwa na maisha ndani ya timu hiyo na hakuwa na furaha kabisa. Lukaku alizua taharuki alipokuwa akifanya…

Read More

ARSENAL V LIVERPOOL YAAHIRISHWA

MCHEZO wa nusu fainali ya Carabao Cup kati ya Arsenal na Liverpool uliopangwa kuchezwa leo Alhamis Januari 6 umeahirishwa kutokana na kuongezeka kwa wimbi la UVIKO-19. Mchezo huo ulipangwa kuchezwa Uwanja wa Emirates ambapo baada ya kuahirishwa utapangiwa siku nyingine. Liverpool ilipeleka maombi yao kwa FA kutaka mchezo huo uahirishwe kutokana na wachezaji wake wengi…

Read More

AUBA AINGIA ANGA ZA NEWCASTLE UNITED

KLABU ya Newcastle United wametuma maombi kwenda Arsenal ili kuipata saini ya mshambuliaji wa klabu hiyo, Pierre-Emerick Aubameyang, 32, katika dirisha hili. Mshambuliaji huyo ambaye huenda asionekane tena uwanjani akiwa na jezi ya Arsenal amekuwa hayupo kwenye kiwango bora tangu msimu huu uanze na katika siku za hivi karibuni amevuliwa unahodha kutokana na vitendo vyake…

Read More

SADIO MANE AREJEA SENEGAL

NYOTA wa kikosi cha Liverpool kinachoshiriki Ligi Kuu England, Sadio Mane na mlinda lango namba moja wa Chelsea Eduardo Mendy wamesafiri pamoja kurejea nyumbani Afrika kwa ajili ya kujiunga na timu ya taifa ya Senegal tayari kwa michuano ya AFCON. Nyota hao walicheza kwenye mchezo wa jumapili wa ligi kuu soka nchini England Chelsea walipowaalika Liverpool. Kwenye mchezo huo uliochezwa Uwanja wa…

Read More

LUKAKU ANAFIKIRIA KURUDI INTER MILAN

MSHAMBULIAJI wa Chelsea, Romelu Lukaku ameweka wazi kuwa kwa sasa hana furaha ndani ya kikosi hicho kinachonolewa na Kocha Mkuu, Thomas Tuchel. Jambo hilo ni kubwa na gumu kwa kuwa linaweza kuvuruga mwendo wa kikosi hicho kwa msimu wa 2021/22. Nyota huyo ameweka wazi kwamba anahitaji kuweza kurejea Inter Milan ili akaendelee na maisha yake…

Read More

NINGECHEZA ZAMA ZA PELE NINGEFUNGA MABAO 3000

MSHAMBULIAJI wa AC Milan, Zlatan Ibrahimovic hajaonesha kukubali uwezo wa mfalme wa Soka kutoka nchini Brazil Pele ambaye anatajwa kuwa ni nyota bora wa muda wote. Licha ya Pele kuzungumzwa kufungwa magoli zaidi ya 1000 katika kipindi cha uchezaji wake, Zlatan haonekani kutishwa na rekodi hizo. “Kama ningecheza enzi za Pele, ningefunga mabao 3000. Hakukuwa…

Read More

MTANZANIA ATUA ULAYA KUBORESHA MISINGI

NYOTA Omary Muvungi kutoka kituo cha mpira wa miguu cha Cambiasso Sports, Omary Mvungi amefanikiwa kwenda nhini Uingereza kwa mwaliko kutoka kwa mchezaji wa zamani wa Chelsea Denis Wise. Nyota huyo ambaye ni mshambuliaji alipata fursa pia ya kupiga picha na mchezaji huyo na nahodha wa zamani wa Chelsea, Dennis Wise baada ya kutua nchini…

Read More

TORRES NI MALI YA BARCELONA

Nyota wa kimataifa wa Hispania Ferran Torres amekamilisha dili lake la kujiunga na FC Barcelona akitokea Manchester City dili linalotajwa kuwa na thamani ya pauni milioni 61. Torres mwenye umri wa miaka 21, anarejea Hispania baada ya miezi 18 tangia aondoke Valencia na kujiunga na Manchester City ambapo sasa ameingia mkataba wa miaka sita (2027)…

Read More