MICHAEL Oliver mwamuzi wa kati atakuwa kati leo kwenye mchezo wa nusu fainali ya Kombe la FA ambalo ni taji la pili kwa ukubwa kwa timu hizo kugombea kando ya ligi.
Itakuwa ni Uwanja wa Wembley saa 11:30 mchezo huo unatarajiwa kuchezwa ikiwa zimepita siku 7 tangu wababe hao wakutane Jumapili iliyopita katika mchezo wa ligi na walitoshana nguvu kwa kufungana mabao 2-2.
Mwamuzi huyua mwenye miaka 37 anasifika kuwa mwepesi kumwaga kadi kwa timu yoyote ile na mpaka sasa ametoa kadi 128 za njano na zile nyekundu 8.
Alikuwa mwamuzi wakati Manchester City ikishinda mabao 4-1 mbele ya Manchester United kwenye Manchester Derby Uwanja wa Etihad huku Liverpool wakishinda mabao 6-0 Leeds United Uwanja wa Anfield
Curacao's players pose for a team photo before the start of the World Cup qualifier football match between Jamaica and Curacao at the National Stadium in Kingston, Jamaica on November 18, 2025. (Photo by Ricardo Makyn / AFP) (Photo by RICARDO MAKYN/AFP via Getty Images)