>

TANZIA:BEKI SONSO ATANGULIA MBELE ZA HAKI

ALLY Mtoni, ‘Sonso’ beki wa mpira aliyekuwa anakipiga ndani ya kikosi cha Ruvu Shooting ametangulia mbele za haki.

Taarifa ambayo imetolewa leo imeeleza kuwa beki huyo amepatwa na umauti kutokana na kusumbuliwa na tatizo la mguu.

Ikumbukwe kwamba Sonso mwenye miaka 29 aliwahi kucheza ndani ya kikosi cha Yanga kisha akaibukia Kagera Sugar.

Timu nyingine ambayo amewahi kucheza na Lipuli ambayo iliwahi kutinga hatua ya fainali ya Kombe la Shirikisho na kupoteza kwa kufungwa bao 1-0 dhidi ya Azam FC.

Pumzika kwa Amani Sonso.