Dodoma Jiji FC vs Yanga SC kinawaka

Dodoma Jiji FC vs Yanga SC kinawaka kesho Mei 13, 2026 Uwanja wa Airtel Singida ambapo kila timu inapambania pointi tatu muhimu.

Yanga SC ni timu pekee ambayo haijapoteza mchezo ndani ya ligi namba nne kwa ubora inakutana na Dodoma Jiji FC ambayo imepoteza jumla ya mechi 7.

Mlinda mlango wa Dodoma Jiji FC, Hussen Masalanga ameweka wazi kuwa wapo tayari kwa mchezo huo na wanawaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi.

“Kwa niaba ya Wachezaji wenzangu tumejiandaa vizuri na mchezo wa kesho na kila mmoja wetu anajua umuhimu wake. Kwa sasa lengo letu ni kuhakikisha tunashinda kila mchezo.

Mashabiki wetu wamekuwa msaada mkubwa sana msimu mzima. Tunahitaji sauti yao, nguvu yao na sapoti yao katika kila mchezo. Tunawaomba wajitokeze kwa wingi kesho ili kutupa nguvu ya kupambana na kupata ushindi.”

Yanga SC ipo nafasi 1 kwenye msimamo na pointi 54, Dodoma Jiji FC nafasi ya 8 na pointi 29 mchezo unatarajiwa kuchezwa saa 10:15 jioni.

***

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu.  Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.

Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.